Tafuta

2022.05.02 'Mater Ecclesiae' 'Mama wa Kanisa' 2022.05.02 'Mater Ecclesiae' 'Mama wa Kanisa'  

Mwezi wa Maria katika Kanisa Kuu la Kipapa

Kila Jumatano za mwezi Mei kuanzia saa 10 kamili jioni katika mwanzo wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro,kutakuwa na sala ya mzunguko ambayo itagusa uwakilishi mkuu wa wakfu kwa Bikira Maria "Mater Ecclesiae.Sala itamalizika saa 11.00 jioni kwa adhimisho la Misa Takatifu.Kila Jumamosi jioni,kwa mwezi Mei,kuanza saa 3 hadi 4.00 usiku kutafanyika maandamano na mishumaa katika uwanja wa Mtakatifu Pietro na picha ya “Mater Ecclesiae”

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Katika fursa ya Mwezi  Mei, ambapo Watu wa Mungu hujikita kwa namna ya pekee kwa ibada ya Bikira Maria, Vikarieti ya Vatican na Parokia ya Mtakatifu Petro inaanzaa mfululizo wa matukio ya kuadhimisha  ibada ya Bikira Maria ambaye anaheshimiwa katika Kanisa Kuu kwa jina la: “Mater Ecclesiae”, yaani mama wa Kanisa. Kwa njia hiyo kila Jumatano za Mwezi Mei saa 10: 00  jioni  kuanzia mwanzoni mwa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, kutakuwa na sala ya mzunguko ambayo itagusa uwakilishi mkuu wa wakfu kwa Bikira Maria. Sala hiyo itamalizika saa 11.00 jioni kwa adhimisho la Misa Takatifu

Na kila Jumamosi jioni, kwa mwezi wote wa Mei, kuanzia saa 3.00 usiku hadi saa 4.00 kutafanyika maandamano na mishumaa mikubwa katika uwanja wa Mtakatifu Pietro wakiwa na picha ya “Mater Ecclesiae”, yaani Mama wa Kanisa  akisindikiza sala ya Rosari Takatifu itakayoongozwa na Kardinali  Angelo Comastri. Picha ya “Mater Ecclesiae” imechotwa juu ya nguzo ya kizamani ya Kanisa Kuu la Kostantini na ilikuwa ndiyo hiyo kabla ya Mtakatifu Paolo VI kutoa jina jipya kwa ajili ya Mtakatifu Petro na kwa ajili ya Kanisa la ulimwengu.

Liturujia inawaita mitume wa Kristo nguzo na msingi wa Kanisa, ikirejea maono ya Yerusalemu ya mbinguni iliyoelezwa katika kitabu cha  Ufunuo. Na Mtakatifu Yohane Paulo II, mnamo 1981, miezi michache baada ya kushambuliwa, alibariki picha hiyo (mosaic) yenye jina la  “Mater Ecclesiae” akionesha shauku kwamba kwa wale watakaokuja kwenye Uwanja huo wa Mtakatifu Petro waweze kuinua mtazamo wao kuelekeza Yeye   kwa kumpati  hisia za uaminifu wa kitoto, salamu binafsi  na sala zao binafsi.

02 May 2022, 17:02