Papa Pio XI:Februari 6,1922 alichauguliwa Kardina Ratti kuwa Papa!
Na Angella Rwezaula – Vatican.
Ilikuwa ni mnamo tarehe 6 Februari 2022 alipochaguliwa Kardinali Achille Ratti na kuchagua jina la Pio XI, na kwa maana hiyo tarehe 6 Februari 2022, ilikuwa ni miaka 100, tangu achagulie Papa kutoka Mkoa wa Lombardia nchini Italia. Kwa jina la ubatizo alikuwa ni Ambrogio Damiano Achille Ratti, baadaye kuwa Pio XI, alizaliwa huko Desio (Milano) tarehe 31 Mei 1857, akiwa ni mtoto wa nne wa Francesco na mama Teresa Galli. Alielimisha kwanye miaka ya utoto na Padre Giuseppe Volontieri, msimamizi wa Kikanisa cha Shirika Upendo desiana kwa sababu walikuwa wamefungua kozi karibu na kwao na akaanza shule za msingi za Seregno tangu 1863 hadi 1866. Mnamo 5 novemba 1867, Achille alijiunga na Seminari ya Mtakatifu Petro shaidi huko Seveso. Baadaye seminari Kuu ya Milano 1875-1876 kwa maka 3 ya kwnza ya Taalimungu na mingine ya mwisho (1878-1879) Matakatifu Pietro shaidi huko Seveso. Baadaye kijana Achille manamo Octoba 187,9 alihamishiwa katika Seminari ya Kipapa ya Lombardo jijini Roma. Miezi miwili baadaye tarehe 20 Desemba 1879, akapaewa daraja la upadre katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yohane huko Laterano.
Wakati huo mnamo tarehe 13 Machi katika Kitivo ha Chuo Kikuu La Spienza akapewa shahada ya Taalimungu na mwaka huo huo tarehe 9 Juni katika Chuo Kikuu cha Gregoriana, akapewa shahada ya sheria za kanoni na 23 Juni katika Chuo Kikuu cha Kipapa cha Mtakatifu Tomasi, shahada ya falsafa. Baada ya kumaliza masomo alirudi Milano na aliitwa Roma mnamo Februari 1912 na Papa Pio X kama makamu mkuu wa Maktaba ya Vatican, na baadaye akawa mkuu mnamo Mosi Septemba 1914. Licha ya ugumu wakati ule uliosababishwa na Vita vya Kwanza vya Ulimwengu vilivyotangazwa na Austria-Hungari dhidi ya Serbia mnamo 28 Julai 1914 na kutoka Ujerumani dhidi ya Urusi tarehe 1 Agosti iliyofuata, mkutubi Achille Ratti (aliinuliwa hadi kuwa na hadhi ya Mkanoni wa Sheria wa Vatican na mtunza Itifaki za Kitume) alipewa sifa hiyo kutokana na ujuzi wake wa kipekee wa kiutamaduni na umahiri wake wa kitaaluma uliounganishwa kwa Maktaba ya Vatican kwa kuunganisha orodha mbalimbali za machapisho ya mati, kuendelea kuorodhesha hati, kukuza toleo la picha la Jiografia ya Tolomeo na kuongeza baraza la urekebishaji.
Ghafla analazimika kukatiza kazi yake kama mtunza maktaba. Kwani mnamo Mei 1918, Papa Benedikto XV, alipomwona kuwa ni mtu sahihi, na alimtuma Poland na Lithuania, akiwa amepewa jukumu la kuwa mwakilishi wa Kitume wa Vatican , na kazi ya kurejesha hali ya shida ya Kanisa katika nchi hizo. Kujitolea bila kukata tamaa kama ilivyokuwa tabia yake nyeti alijaribu kufufua ulimwengu huo mkubwa wa Kikatoliki, uliochoshwa na vita, miaka minne ya uvamizi wa Wajerumani pamoja na mapambano ya umwagaji damu ya kikanda. Tangu serikali ya Poland kurejesha uhusiano wa kidiplomasia na Vatica , tarehe 3 Julai 1919, Mwakilishi wa Kitume Achille Ratti alithibitishwa kuwa mwakilishi wa mamlaka ya Kipapa kwa cheo cha Balozi wa Vatican na tarehe 28 iliyofuata aliwekwa wakfu wa kuwa Askofu Mkuu katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yohane huko Warsaw, mbele ya Rais wa Jamhuri ya Poland. Lakini mnamo Agosti 1920, Poland ilivamiwa na askari wa Bolshevik. Wanadiplomasia wote wakakimbia, lakini Balozi Achille Ratti alibaki katika wadhifa wake akithibitishwa kwa Padre P. Theissling, aliyekuwa Mkuu wa Shirika la Wadominika, aliyekuwepo siku hizo huko Warsaw: “Ninajua kabisa uzito wa hali hiyo, lakini asubuhi ya leo, nikiadhimisha Misa nilitoa maisha yangu kwa Mungu. Mimi ni kuhani katika hali yoyote” Baadaye, kwa kutii agizo la Benedikto XV, mwishoni mwa mwaka aliondoka Poland na kurudi Italia kuchukua wadhifa wa Askofu Mkuu wa Milano na kuteuliwa kuwa Kardinali.
Kufuatia kifo cha Papa Benedikto XV, mnamo Januari 22, 1922, Makardinali walikutana mnamo tarehe 2 Februari wakiwa ni makadinali 53. Siku nne baadaye, katika kura ya kumi na nne, Kardinali Achille Ratti alichaguliwa kuwa Papa kwa kura 42 (6 zaidi zilizokuwa zinahitajika ). Na alinachagua jina la Pius XI na, kwa ishara kuu aliweza kutoa baraka za kiutamaduni za "Urbi et orbi" kupitia kwenye Ubaraz nje ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro ambao ulikuwa umefungwa tangu Ufalme wa Italia ulipochukua Vatican mnamo 1870. Waamini walikusanyika uwanjani wakishangilia na wakipiga kelele: “Uishi muda mrefu Pio XI! Uishi Italia" . Hiki ni kipindi ambacho lazima kikumbukwe kati ya kile kilichoongoza kufikia suluhisho la suala la Kirumi. Tayari katika Waraka wake wa kwanza wa kitume wa, Ubi arcano wa tarehe 23 Desemba 1922, alirejea juu ya shida: kwamba "Italia haina chochote au italazimika kuogopa kutoka kwa Vatican: Papa, yeyote yule, atarudia kila wakati: Nina mawazo ya amani, si ya dhiki ; mawazo ya amani ya kweli, na kwa hiyo haijatenganishwa na haki, ili kwamba inaweza kusemwa: Haki na amani zimebusu. Ni juu ya Mungu kuleta saa hii na kuifanya isikike; kwa wenye hekima wenye mapenzi mema usiiache iende bure; itakuwa ni kati ya saa zito na zenye matunda mengi kwa ajili ya kurejeshwa kwa Ufalme wa Kristo na kwa ajili ya kutuliza Italia na dunia.”
Katika Waraka wake wa Divini illius Magistri wa tarehe 31 Desemba, 1929, Papa Pio XI anadai kwamba Kanisa na familia lina haki msingi ya kuelimisha vijana:haki isiyoweza kukiukwa inayotangulia ile ya Serikali. Elimu inayotamaniwa na Kanisa ina lengo sahihi na la haraka la kushirikiana na neema ya Mungu kuunda Mkristo wa kweli na mkamilifu. “Hatupaswi kamwe kupoteza mtazamo wa ukweli kwamba somo la elimu ya Kikristo ni mwanadamu kwa ujumla, roho iliyounganishwa na mwili katika umoja wa asili, katika uwezo wake wote, wa asili na usio wa kawaida, ambayo tunajua na sababu sahihi na Ufunuo: kwamba ni, mwanadamu ambaye ameanguka kutoka katika hali ya asili, lakini alikombolewa na Kristo na kuunganishwa tena katika hali isiyo ya kawaida ya mwana wa kupitishwa wa Mungu, ingawa si katika mapendeleo ya kabla ya asili ya kutokufa kwa mwili na uadilifu au usawa wa mwelekeo wake.
Katika waraka wake wa Kitume wa Casti connubii wa tarehe Desemba 1930, akirejea katika Waraka wa Arcanum Divinae ya Papa Leo XIII ya tarehe 10 Februari 1880, Papa Pio XI analaani upagani mamboleo ambao, kwa kuunga mkono ukombozi rasmi wa wanawake, kwa hakika unadhoofisha familia iliyounganishwa na Mungu katika umoja wa ndoa. “Jinsi hadhi ya ndoa iliyo safi ilivyo kubwa, tunaweza kutambua hasa kutokana na kile ambacho Bwana Wetu Yesu Kristo, Mwana wa Baba wa Milele, alipotwaa asili ya mwanadamu aliyeanguka, katika uchumi ule wenye upendo mwingi zaidi ambao alifanya nao malipo kamili binadamu wetu, si tu alitaka kuelewa kwa namna fulani kanuni hii na msingi wa jamii ya ndani na kwa hiyo ya muungano wa binadamu, lakini pia kukumbuka juu ya usafi wa kwanza wa taasisi ya kimungu, na kuinua kiukweli na sakramenti kuu mpya . Sheria, hivyo kuikabidhi nidhamu yake yote na kulitunza Kanisa mchumba wake”.
Katika mwaka wa waraka wake Quadragesimo wa tarehe 15 Mei 1931, Papa Pio XI alisherehekea, nakufafanua akiunganisha mkono Waraka wa Rerum novarum wa Papa Leo XIII uliochapishwa mnamo tarehe 15 Mei 1891, akionesha kwa uchanganuzi katika uhusiano kati ya makampuni na wafanyakazi kwamba utata mkubwa wa mafundisho ambayo ni sifa ya Ukatoliki wa kijamii. . “Kwa maana hiyo, kwa kuwa utaratibu wa kisasa wa uchumi umeegemezwa hasa juu ya mtaji na kazi, kanuni za akili sahihi, yaani, za falsafa ya kijamii ya Kikristo, kuhusu mambo mawili yaliyotajwa na mahusiano yao lazima yajulikane na kutekelezwa. Kwa njia hiyo, ili kuepusha kukithiri kwa ubinafsi kwa upande mmoja, na vile vile ujamaa kwa upande mwingine, mtu lazima zaidi ya yote azingatie asili ya pande mbili, ya mtu binafsi na ya kijamii, ya mtaji au mali, na ya wafanyakazi” .
Katika Waraka wake Ad Catholici sacerdotii wa tarehe 20 Desemba 1935, Papa Pio XI anatukuza ukuhani wa Kikatoliki na utume wake wa kutoa huduma ulimwenguni. “Padre, kwa wito na mamlaka ya kimungu, ndiye mtume mkuu na mhasishahji asiyechoka wa elimu ya Kikristo ya vijana; kuhani kwa jina la Mungu hubariki ndoa ya Kikristo na kutetea utakatifu wake na kutoweza kufutwa dhidi ya mashambulizi na mikengeuko inayopendekezwa na uchoyo na uasherati; kuhani anatoa mchango halali zaidi katika utatuzi au angalau kupunguza migogoro ya kijamii, akihubiri udugu wa Kikristo, akikumbusha kila mtu wajibu wa pande zote wa haki na upendo wa kiinjili, kutuliza roho zilizokasirishwa na shida za kiadili na kiuchumi, akielekeza kwa matajiri na mapendo, maskini ambao ni wema pekee aambao kila mtu anaweza na lazima atamani.
Tayari mnamo 1926, wakati Wakatoliki walipoteswa vibaya sana huko Mexico, alisimama kidete mnamo Novemba 18 na waraka wake Iniquis afflictisque akilaani hali hiyo kubwa: “ Ikiwa katika karen za kwanza za Kanisa na katika nyakati nyingine zilizofuta waliwatendea wakatisto kwa namna mbaya sana labda haikutokea mahali popote kwamba, kwa kukanyaga na kukiuka haki za Mungu na za Kanisa, idadi ndogo ya watu, bila kujali utukufu wa mababu zao, bila huruma kwa raia wenzao, wakaminya kwa kila njia uhuru wa wengi wenye viungo hivyo na sanaa iliyotafakariwa sana, na kuongeza mfano wa sheria ili kuficha jeuri”. Lawama kama hizo za mateso ya mara kwa mara ya Wamexico zinaoneshwa kwa nguvu na Papa pamoja na Waraka wa Acerba animi wa tarehe 29 Septemba 1932 na Fermissimam constantiam ya tarehe 28 Machi 1937: Jaribio lilifanywa kugonga katika hatua muhimu ya Kanisa: uwepo wa makasisi na uongozi wa Kikatoliki, katika jaribio la kuwaondoa hatua kwa hatua kutoka katika Jamhuri. Tukikabiliwa na shutuma za mara kwa mara zinazotolewa kwa Kanisa kwamba halijali matatizo ya kijamii, au haliwezi kuyatatua, hatupaswi kujiepusha na kutangaza kwamba ni mafundisho na kazi ya Kanisa tu, ikisaidiwa na Mwanzilishi wake wa Kimungu ili kurekebisha maovu makubwa sana yanayowatesa wanadamu”.
Bila shaka, uingiliaji kati ambao Papa Pio XI alilazimika kutekeleza tarehe 29 Juni 1931 na Waraka wake Non abbiamo bisogno yaani “Hatuhitaji” , kuhusiana na serikali ya Italia ni ngumu, ambayo, kwa shinikizo la wanamsimamo mkali wa kifashisti, ilivunja vyama vya vijana na vyuo vikuu vya Wakatoliki. Ingawa na kitendo hicho Papa bado alifurahia nuru iliyotokana na Makubaliano yaliyokuwa yamefanyika ya Mkataba wa Latera uliotiwa saini mnamo tarehe 11 Februari 1929 (mwanga, zaidi ya hayo, ambao ulikuwa umepingwa tangu wakati huo na watu wachache wa kidunia hadi mwisho), pamoja na hayo hakosi maneno ya kutoa manung’uniko na kukemea kwa ukali na vurugu, hadi kupigwa na damu, na kutoheshimu vyombo vya habari, neno na tendo, dhidi ya mambo na watu, bila kuwatenga ambayo ilitangulia, na kufuatiwa utekelezaji wa hatua ya ghafla ya polisi, ambayo mara nyingi ujinga au bidii mbaya ilienea kwa vyama na vyombo kwa walioathiriwa na maamrisho ya hali ya juu, hadi kwenye hotuba za watoto wadogo na mashirika ya Binti wa Maria.
Na kwa Waraka wa Dilectissima Nobis wa tarehe 3 Juni 1933, papa Pio XI alipinga vikali kwamba “Sasa hatuwezi kushindwa kupaza sauti zetu tena dhidi ya sheria, iliyoidhinishwa juu ya maungamo ya kidini na makutano, ambayo ni kosa jipya na kubwa zaidi, sio tu kwa dini na kwa Kanisa, lakini pia kwa kanuni zinazodaiwa za uhuru wa raia ambayo inatangaza Utawala mpya wa Uhispania kuwa msingi ». ... “Kwa yale tuliyoyaeleza, ni dhahiri ... kwamba mapambano yanayofanywa dhidi ya Kanisa nchini Hispania, badala ya kutoelewa imani ya Kikatoliki na taasisi zake zenye manufaa, lazima yachangiwe na chuki inayokuza madhehebu yanayopotosha. Bwana na Kristo wake kila mpangilio wa kidini na kijamii, kwa bahati mbaya tunaona yakitokea Mexico na Urusi “ Mnamo 1937, wakati ilionekana kushinda mipaka yote ya uvumilivu wa kidiplomasia Papa , Pio XI aliingilia kati kwa Nyaraka mbili zenye nguvu: mnamo tarehe 14 Machi 14 na Mit brennender Sorge (Akiwa na wasiwasi hai) dhidi ya Reich ya Kiazi na mnamo tarehe 9 Machi na Divini Redemptoris dhidi ya ukomunisti wa wasioamini huko Urusi. Akilaani bila ubishi upagani mamboleo wa Ujerumani, Papa Pio XI alithibitisha kwamba “hata katika siku zijazo hatutachoka kuzishutumu mamlaka zinazohusika kwa uwazi kwa uharamu wa hatua za vurugu zilizochukuliwa hadi sasa, na wajibu wa kuruhusu udhihirisho huru wa utashi”.
Kuhani katika maana pana ya neno hili, Papa Pio XI alijishughulisha na kuongezeka kwa shughuli za kimisionari, kwa kuwaweka wakfu Maaskofu sita wa Kichina katika Kanisa la Mtakatifu Petro mnamo tarehe 28 Oktoba 1926 (rejea homilia Iam finis) na baadaye Maaskofu wengine wa kiasili; alijitolea kuyafanya matatizo ya Makanisa ya Mashariki yajulikane na kutiliwa maanani; alijitoa kwa ari na usadikisho kwa malezi na utakatifu wa wakleri; alitoa msukumo mkubwa kwa ajili ya masomo ya kibinadamu na kuimarisha sanaa takatifu; alihamasisha Jubilei tatu zilizokaribishwa kwa ushiriki mkubwa sana wa Ukatoliki. Utambuzi maalum umehifadhiwa wa Papa Pio XI na ulimwengu wa mawasiliano ya kijamii. Ilikuwa tarehe 12 Februari 1931, katika kumbukumbu ya miaka tisa ya kuwekwa wakfu kwake, kwa kuwakilishwa na Guglielmo Marconi, alizindua kituo chenye nguvu cha Radio Vatican, kwa kutuma ujumbe Qui arcano Dei kwa kila mtu katika lugha ya Kilatino. Hati hiyo ya kihistoria inashughulikiwa hasa na Pio XI, Papa wa Kanisa la Ulimwengu wote, “kwa viumbe vyote, Mungu, Wakatoliki, viongozi, wataa, wamisionari, waamini wote, wapagani na wapinzani, watawala, raia, matajiri, maskini, wafanyakazi na waajiri, wanaoteswa na kuteswa”. Papa baadaye alitumia huduma ya Radio ya kisasa katika nyakati nyinginezo katika miaka iliyofuata, kutuma ujumbe kwa wasiklizaji walio mbali, kumshukuru Guglielmo Marconi ambaye mnamo tarehe 11 Februari 1933 pia aliweka upatikanaji wa kituo cha radio cha mawimbi mafupi zaidi, kinachofafanuliwa na Papa kama matumizi ya ubora wa kisayansi.
Akiwa ameugua sana mnamo Januari 1939, Papa Achille Ratti , yaani Papa Pio XI, aliaga dunia tarehe 10 iliyofuata Februari, usiku wa kuamkia mwaka wa kumi na saba wa upapa wake. Masalia yake yapo kwenye Makaburi ya Vatican , karibu na makaburi ya Papa Benedikto XV na Pio X. Sauti ambayo kabla ya kifo chake alikuwa akitayarisha Hati dhidi ya ubaguzi wa rangi na utawala wa kifashisti haikupata uthibitisho. Nakala ya hotuba ya mwisho isiyokamilika ya Pio XI, ambayo ilibaki bila kuchapishwa kwa muda mrefu, ilijulikana tu na Papa Yohane XXIII mnamo tarehe 6 Februari 1959. Na baadaye ikachapishwa mwishoni mwa kitabu kilichofuata ambacho kiliwekwa kwa ajili ya kufafanua maisha ya Papa Ratti, yaani papa Pio XI. Tukikumbuka utendaji wa kidini wa Papa Ratti, ni muhimu kukumbuka kwamba katika kipindi kirefu cha upapa wake aliwatangaza Yohane Fisher (1469-1535) na Thomas More (1478-1535) kuwa watakatifu, waathirika wa mifarakano ya Mflame Henry VIII; Yohane Bosco (1815-1888), mwanzilishi wa Shirika la Kisalesians na Teresa wa Mtoto Yesu (1873-1897), mfano wa usahili na upendo. Kwa kuongezea, Albert Mkuu (1193-1280), Pietro Canisio (1521-1597),Yohane wa Msalaba (1542-1591)na Roberto Bellarmino (1542-1621)walitangaza Madaktari wa Kanisa. Lakini bila kupuuza hatua ya ujasiri, pia ya kisiasa, ambayo Papa Pio XI aliifanya kutetea maadili ya lazima ya Kikristo.