Tafuta

Pope Francisko na Rais Borut Pahor  wa Slovenia, mjini Vatican. Pope Francisko na Rais Borut Pahor wa Slovenia, mjini Vatican. 

Papa amekutana na Bw.Borut Pahor,rais wa Jamhuri ya Slovenia

Katika mazungumzo kati ya Baba Mtakatifu na mgeni wake,na viongozi wengine wa Vatican,wameridhishwa na uhusiano wa kidiplomasia uliopo kati ya nchi hizo mbili ndani ya miaka 30 na kupongezana juu ya mazungumzo yaliyopo katika Kanisa na Mamlaka ya raia nchini Slovenia.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Baba Mtakatifu Francisko, Jumatatu tarehe 7 Februari 2022 amekutana na kuzungumza na Rais Borut Pahor, wa Jumhuri ya Slovenia, na aliosindikizana nao. Baada ya Mkutano huo pia amekutana na Katibu wa Vatican, Kardinali Pietro Parolin akiambata na Askofu mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu mkuu wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa Kimataifa, Vatican.

Papa amekutana na Rais wa Slovenia Bwana Borut  Pahor
Papa amekutana na Rais wa Slovenia Bwana Borut Pahor

Katika mazungumzo kati yao na mgeni huyo wameridhishwa na uhusiano wa kidiplomasia uliopo kati ya nchi hizi mbili ndani ya mzunguko wa miakatherathini tangu kuufungua na kupongezana juu ya mazungumzo yaliyopo katika Kanisa na Mamlaka ya raia nchini Slovenia.

 Rais wa Slovenia Bwana Borut  Pahor akiwa na mkutano na Makatibu wa Vatican
Rais wa Slovenia Bwana Borut Pahor akiwa na mkutano na Makatibu wa Vatican
 Rais wa Slovenia Bwana Borut  Pahor akiwa na mkutano na Makatibu wa Vatican
Rais wa Slovenia Bwana Borut Pahor akiwa na mkutano na Makatibu wa Vatican

Wakiendelea na mchakato wa mazungumzo yao kati ya Rais Borut Pahor na viongozi wakuu wa Vatican, wametazama pia masuala ya kimataifa na kikanda, miongoni ni pamoja na ushirikiano wa kikanda, upanuaji wa uanachama wa  Umoja wa Ulaya katika Nchi za Mashariki ya Ulaya na hali halisi inayoendelea nchini Ukraine.

Papa na  Rais wa Slovenia Bwana Borut  Pahor
Papa na Rais wa Slovenia Bwana Borut Pahor
07 Februari 2022, 15:26