Tafuta

2021.10.07 Papa Francisko na Angela Merkel, Kansela wa Jamhiri ya Shirikisho la Ujerumani. 2021.10.07 Papa Francisko na Angela Merkel, Kansela wa Jamhiri ya Shirikisho la Ujerumani. 

Mkutano wa Papa na Kansela Angela Merkel

Alhamisi Oktoba 7,2021,Papa Francisko amekutana na Kansela wa Ujerumani.Kitovu cha mazungumzo yao kilikiwa ni janga la uviko na uhamiaji.

Na  Sr. Angela Rwezaula – Vatican.

Baba Mtakatifu, Alhamisi tarehe 7 Oktoba 2021, asubuhi alikutana na Kansela wa Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani Angela Merkel, ambaye baadaye alikutana na Kardinali Pietro Parolin, Katibu wa Vatican akiambatana na Askofu Mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu wa Mahusiano na ushirikiano na  Mataifa.

Katika mazungumzo yao wameonesha kupongezana juu ya mahusiano mema yaliyopo kati ya nchi hizi mbili na matunda ya ushirikiano kati ya Vatican na Ujerumani kwa mujibu wa maelezo ya Msemaji wa vyombo vya habari Vatican.

Mazungumzo ya Papa na Kansela Angela wakati wa Mkutano wao
Mazungumzo ya Papa na Kansela Angela wakati wa Mkutano wao

Baadaye amegusia masuala yanayowahusu wote katika muktadha wa kimataifa na kikanda, wamejikita kuona fursa za kuzindua  kwa ushirikiano kwa ajili ya kukabiliana na mgogoro mkubwa unaoendelea kwa namna ya pekee juu ya matokeo mabaya ya dharurua ya kiafya na uhamiaji.

Kibadilishana zawadi
Kibadilishana zawadi

Katika kubadlishana zwadi, Papa Francisko ametoa zawadi ya Picha ya shaba inayoonesha Mlango mtakatifu, Kitabu kikubwa chenye mkusanyo wa  hati za Papa, Ujumbe wa Amani ya Mwaka na Hati juu ya Udugu wa Kibinadamu. Na zawadi kwa upande wake Kansela wa Ujerumani Merkel, amempatia Papa Tafakari ya Injili za Dominika za vitabu vitatu, Kitabu kikubwa cha Michelangelo na bidhaa nyingine za vyakula.

08 October 2021, 16:10