Ziara ya kitume ya Papa Francisko nchini Hungaria: Eneo la tukio liko tayari. Ziara ya kitume ya Papa Francisko nchini Hungaria: Eneo la tukio liko tayari. 

Hija ya kitume nchini Hungaria na Slovakia:ni safari ya kiroho

Kwa mujibu wa msemaji wa vyombo vya habati Dk Bruni amewakilisha ziara ya 34 ya Upapa tarehe 12-15 Septemba ijayo:huko Budpest hija ni kwa ajili ya kuheshimu Sakramenti,epuka kuchanganya mambo mengine zaidi ya kiroho.Nchini Slovakia ni kuwatia moyo watu waliojeruhiwa na utawala wa mabavu.Afya ya Baba Mtakatifu inaendelea vizuri.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican.

Katika ziara ya kitume ya 34 kimataifa ya Papa Francisko ambayo inajumuisha nchi 54 alizotembelea duniani inataka kuwa hija katika moyo wa Ulaya, wakati ambapo Papa atakabiliana na mada ambazo zinahusiana ndani ya bara. Lakini zaidi, ziara hii inataka kuwa ya kiroho, itakayo anza na kuabudi Ekaristina kuhitimisha kwa sala ya Bikira Maria wa Mateso ambaye hakuacha kamwe kutoa ulinzi na msaada wake kwa watu huko waliojeruhia na utawala wa mabavu. Hayo ndiyo kwa ufupi wa msemaji wa Vyombo vaya habari Vatican, Dk. Matteo Bruni, akifafanua juu ya siku nne ambazo Papa Francisko atakuwa nazo kuanzia tarehe 12 hadi 15 Septemba ijayo.

kONGAMANO LA EKARISTI HUKO BUDAPEST
kONGAMANO LA EKARISTI HUKO BUDAPEST

Baba Mtakatifu kwanza anatua jijini Budapest kuadhimisha misa takatifu ya kufungwa kwa Kongamano la Ekaristi kimataifa na baada kueleka nchini Slovakia kwa akisimama katika  vituo vya mji mkuu Bratislava na miji mingine mitatu: Prešov, Košice na Šaštin. Ni ziara kwa hakika ya kiroho, kwa maana hiyo ni vema kuepuka ,kuchanganya mambo mengine zaidi ya yale ya kiroho, kwa mujibu wa Dk Bruni, wakati anaijibu baadhi ya masali ya waandishi wa habari waliunganika katika ukumbi  wa habari Vatican, kwa ajili ya mkutano wa kuwakilisha ziara hiyo. Maswali hayo zaidi yalilenga hasa juu ya mkutano wa Papa na Waziri Mkuu Viktor Orbán Jumapili asubuhi kabla ya Misa katika Uwanja wa Mashujaa. “Ni mkutano na mamlaka ya juu nchini, na ni wazi kati ya hawa pia kuna Orban”, alisema Dk Bruni, akielezea kuwa “uwepo wa waziri mkuu na familia yake kwenye Misa ya kipapa “utathibitishwa na watu wa Hungaria”.

Hija kwa heshima ya Ekaristi

Ni hija kwa heshima ya Sakramenti Takatifu, alisema msemaji wa Vatican, akikumbuka kwamba mwanzo wa safari hii unaweza kufuatwa tena na hamu ya Papa ya kuwa karibu na mamia ya wanaume na wanawake ambao, tangu Jumapili iliyopita, walianza kushiriki Kongamano la Ekaristi. Hata hivyo nchini Hungaria ilifungua milango yake kuelekea Slovakia, alikumbusha Dk. Bruni. Papa mwenyewe, katika mkutano na waandishi wa habari juu ya safari ya kurudi kutoka Iraq, mnamo Machi, akifunua mchakato wa ndani unaoambatana na uchaguzi wa maeneo ya kutembelea, na ambayo alikuwa ameelezea kwamba alishauriwa na mmoja wa washirika wake wa karibu kutazama hata Budapest na kuelekea Bratislava kwa sababu ni masaa mawili kwa gari.

Hatua ufupi ya kudhaniwa ambayo badala yake ilibadilika kuwa safari ya masaa sabini na mbili katika miji mikuu ya eneo hili la Ulaya ya Kati Mashariki, ambayo mengi ya hayo Mtakatifu Yohane Paulo II alikuwa tayari ametembelea wakati wa safari tatu: mnamo 1990, 1995 na 2003, miaka miwili kabla ya kifo chake. Halafu kutoka sehemu ya Papa Wojtyla kulikuwa na mwaliko kwa Kanisa na kwa jumuiya za Kikristo kushiriki katika ujenzi wa jamii ambayo ilikuwa ikiongezeka polepole kutoka katika  vitisho vya kinazi na kutoka kwa “makosa na mateso” ya utawala wa kikomunisti. Hali hakika ni tofauti na ile ya PapaFrancesco ambayo atakutana nayo wiki ijayo. Walakini, watu na ardhi ni sawa na majeraha ya miaka hiyo ya giza bado vina uzito mkubwa katika roho za wanaume na wanawake wengi. Papa anawatembelea watu ambao wamepata utawala kandamizi wa imani na uhuru wa kidini, pamoja na maaskofu, mapadre, watawa, watu walei waliofungwa, kuteswa, kuuawa shahidi, makuhani walibaki kwa siri katika viwanda ambavyo waliajiriwa, lakini pia Wakristo wanajivunia kuoinga na,wakati mwingine hadi kufikia damu, uovu na mateso”.

Hatua za usafi baada ya operesheni

Mbali na matukio na mada za safari hiyo, Dk. Matteo Bruni pia alijibu maswali ya waandishi wa habari juu ya hatua zozote maalum za kiafya zilizopangwa wakati wa safari, kufuatia upasuaji wa utumbo wa Papa hivi karibuni mnamo Julai 4: “Hakuna hatua maalum, lakini tahadhari ya kawaida. Kama kawaida, kuna daktari na wauguzi wengine kwenye bodi,2 alisema. Na kwenye bodi, katika msafara wa Papa, wakuu wa Sekretarieti ya Nchi watakuwepo: Kardinali Pietro Parolin, Katibu wa Jimbo; naibu Askofu Mkuu Edgar Peña Parra na Katibu wa Mahusiano na Mataifa, Askofu Mkuu Paul Richard Gallagher. Kadinali pia watakuwapo Kardinali Leonardo Sandri, rais wa Baraza la Kipapa la  Makanisa ya Mashariki, na Kardinali Miguel Ángel Ayuso Guixot, rais wa Baraza la Kipapa la Mazungumzo ya Kidini. Kama utamaduni baadaye pia atakuwa mfanyakazi wa Vatican, wakati huu mfanyakazi wa Serikali ya Vatican.

Vizuizi vya Kupambana na Covid

Kama kwa hatua dhidi ya Covid wakati wa safari (kulingana na data isiyo rasmi, kuna visa 200 vya maambukizi kwa siku nchini Slovakia), na hasa kukomeshwa kwa jukumu la kupitisha kadi ya kijani ili kushiriki katika sherehe za Kipapa, Bruni alifafanua: Haya ni maamuzi ya serikali mahalia , ninaweza kufikiria kwamba wamechukua hatua zote muhimu”.

11 September 2021, 11:09