Vatican:Jezi za wawakilishi wa mchezo kwa wafanyakazi Vatican zinauzwa
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican.
Inawezekana hatimaye kununua kupitia majumba ya makumbusho na duka la nguo katika katika serikali ya mji wa Vatican, jezi rasimi ya uwakilishi wa michezo kwa mpira wa miguu, kwa wafanyakazi wa Vatican. Yote hayo yamewezekana, shukrani kwa kazi kubwa ya Viongozi wa Chama ,lakini hasa kwa kuangazwa mmoja wa wakuu hao ambaye wakati wa janga la Uviko-19 alifikiria kuzindua changamoto hii nzuri!
Ni seti nzima ikiwa na mfuko pia kofia rasimi, ambapo fedha zitakazopatikana zitakwenda kwenye Mfuko wa upendo wa kitume wa Papa kwa ajili ya wenye kuhitaji zaidi.
Wazo hili hata hivyo limekutana na hamu kubwa ya wengi. Mtu wa kwanza kupokea zawadi hii ya jezi namba moja ni Papa Francisko ambaye aliipokea tangu tarehe 23 Juni 2021 wakati wa kumaliza katekesi yake. Ukabidhishwaji wa jezi hizi rasimi kama zawadi kwa makardinali, maaskofu na wakurugenzi mbali mbali wa Mabaraza ya kipapa umeendelea na bado unaendeleoa kama ishara ya kuonesha shukrani kubwa kwa ajili ya msaada uliopokelewa katika mchakato wa miaka hii na kuonesha hasa utashi wa kuendeleza katika shughuli za michezo, kwa ajili ya ufadhili, urafiki na utumaduni wa mazungumzo na kukutana.
Shughuli za michezo zitaanza mwezi Septemba ujao kwa ushiriki wa Michezo ya karafiki na goli kwa ajili ya Hospitali ya watoto katika hukusanyai wa fedha kwa ajili ya kitengo cha hospitali ya watoto katika mfuko wa Mtakatifu Matayo na mfuko wa Mondini huko Pavia Italia. Itafuata baadye michuano ya mashirika mwengine ya mpira wa mikuu kwa wanaume na wanakea wa Bambino Gesù, kwa kuwania kikombe cha Vatican na kikombe bora cha Vatican, na mwishowe katika Siku ya Familia.