Vatican:watu wengine 300 wamepewa chanjo dhidi ya Covid
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican.
Ombi ambalo lilikuja kwa hiari kutoka kwa watu wengi wanaoishi mitaani, ambalo lilipokelewa kwa ukarimu wa Papa ili kusaidia walio katika mazingira magumu zaidi na pia wale walio wazi zaidi kupata maambukizi ya virusi vya Corona linaendelea kutoa matunda mema. Kardinali Konrad Krajewski, Msimamizi wa Sadaka ya Kitume ya Papa ameeleza jinsi ambavyo tangu wiki mbili katika kliniki ya Mama wa Huruma, iliyoko kwenye nguzo za Mtakatifu Petro, inaendelea kwa dhati kutoa mshikamano wa wale ambao kwa kawaida hawana uwezo wa kupata chanjo kwa haraka.
Kutokana na hilo pia Jumamosi tarehe 8 Mei 2021 watu wengine 300 wamekaribishwa katika Ukumbi wa Paulo VI, Vatican na wapewa chanjo. Hawa ni watu ambao kwa kawaida hawasaidiwi na mashirika yanayofanya kazi katika maeneo ya jiji, kama ilivyotokea katika wiki za hivi karibuni kwa takriban ya watu maskini 1,400 waliopewa chanjo jijini Vatican.
Toa mchango wako katika kampeni ya "chanjo iliyosimamishwa"
Kwa mujibu wa Msimamizi wa Mfuko wa Sadaka ya Kitume, ameelezea vile vile hatua nyingine iliyoanzishwa ya kampeni ya Chanjo iitwayo “ Chanjo iliyosimamishwa”na ambayo imekaribishwa kwa kiasi kikubwa zaidi ya matarajio yote. Kutoa zawadi katika kipindi cha matatizo siyo kitu rahisi, kwani kinahitaji moyo na kwa maana ni thamani msingi na neema ambayo kwa mchango mdogo unaoweza kutolewa unaweza kusaidia wale walio na mahitaji zaidi; na ni shukrani pia kwa mchango wako mdogo, unaweza kutolewa kupitia tovuti: www.elemosineria.va ili uweze kuwa na mshikamano katika ulimwengu unaoendelea kuteseka sana na virusi.
Kwa mfano India, nchi iliyoathiriwa vibaya sana na wimbi la pili la janga na ambalo Papa Francisko ametoa wito wake akionesha ukaribu wake , amepokea dola 200,000 za kuweza kutumika katika vita dhidi ya Covid. Kwa upande wa Sria,ambayyo pia ni nchi nyingine iliyo na mzozo usio na mwisho pia na virusi wa corona, imepokea euro elfu 350. Kwa mujibu wa msimamaizi wa Sadaka ya Kitume ameeleza kuwa michango yote inakabidhiwa katika Ubalozi wa Kitume wa Vatican mahalia ambao baadaye huwasambazia kulingana na mahitaji.
Kushiriki muujiza wa hisani
Mnamo tarehe 23 Aprili 2021 , katika fursa ya sikukuu ya Mtakatifu George na siku ya Somo wa Papa, Baba Mtakatifu Francisko alikuwa amewashangaza watu takriban 600 wanaohitaji ambao walipokea kipimo cha pili cha chanjo ya Pfizer-Biontech. Kiwango cha kwanza kilichukuliwa wakati wa Wiki Takatifu na hivyo kutoa tena wito wa Papa ili pasiwepo mtu aliyetengwa kwenye kampeni ya chanjo dhidi ya virusi vya corona.