2021.05.03 Papa akutana na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Iraq Bwana  Fuad Hussein 2021.05.03 Papa akutana na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Iraq Bwana Fuad Hussein  

Papa akutana na Waziri wa Mambo ya Nchi za Njie Iraq,Fuad Hussei

Katika mazungumzo yao yaliyodumu karibia dakaka 30, kumekuwapo na kumbu kumbu ya ziara ya Papa Francisko mwezi wa tatu uliopita. Papa ametoa shukrani zake kwa makaribisho akiwatakia kila mmoja akue katika mshakamano na uwezo wa kujibambua wawajibikaji udhaifu wa mwingine.

Na Sr. Angela Rwezaula - Vatican.

Kwa mujibu wa msemaji wa Vyombo vya habari Dk. Matteo Bruni kwa waandishi wa habari amethibitisha kuwa Papa Francisko Jumatatu tarehe 3 Mei 2021, amekutana na waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Iraq, Bwana Fouad Hussein.

Wakati wa mazungumzo yao yaliyodumu karibu dakika 30, Baba Mtakatifu amepata wote fursa ya kukumbuka kwa shukrani makaribisho mazuri aliyopata wakati wa ziara yake ya hivi karibuni nchini Iraq iliyofanyika kuanzia tarehe 5 hadi 7 Machi 2021. Na kwa wote  Papa amepyaisha matashi mema kwa kila mmoja i waweze kukua katika mshikamano na wawe na uwzo wa kujitambua kama wahusika wa udhaifu wa mwingine.

 

03 May 2021, 15:29