Kard.Parolin:Ni udharura wa kusitisha ghasia katika mzozo Mashariki ya Kati
Na Sr. Angela Rwezaula - Vatican.
Ni wasi wasi mkubwa wa Papa na Makao makuu Vatican juu ya kile kinachotokea katika Ardhi Takatifu ambapo inazidi kuongezeka kwa vurugu kati ya Israeli na Hamas. Hayo yameelezwa na katibu wa Vatican, Kardinali, Pietro Parolin, kando ya uwasilishaji wa kitabu ambacho wamemkumbuka mkurugenzi wa zamani wa Osservatore Romano, Mario Agnes, kilichosainiwa na mwandishi wa habari Ignazio Ingrao, katika Jumba la Borromeo, ambacho ni kiti cha Ubalozi wa Italia jijini Vatican. Kardinali Parolin amesisitiza udharura wa maafikiano na ameelezea juu ya wasiwasi mkubwa wa hali hii ya ushawishi, ambayo inaendelea licha ya juhudi za jumuiya ya kimataifa ya kutaka kuleta usitishaji wa mapigano hayo.
“Mzozo huo unaleta magofu na vile vile vifo, amesema Kardinali Parolin. Na amekumbuka maneno ya Papa Francisko mra baada ya Sala ya Malkia wa Mbingu siku ya Jumapili tarehe 16 Mei, wakati alipotoa umakini wa ulimwengu hasa juu ya watoto waliokufa. “Wasiwasi wetu ni ule wa Baba Mtakatifu na kujitoa kufanya kila linalowezekana ili kumaliza mzozo huo”, amesema Katibu wa Vatican.
Kardinali Parolin akijibu maswali ya waandishi wa habari ambao waliuliza ikiwa Vatican inaweza kufanya kama mpatanishi wa suala la Israeli na Palestina amejibu kwamba: “Nadhani kuna mtu ameambiwa kwamba hawataki kuingiliwa. Kwa maana ya kiufundi labda sio, na sidhani kama ni sawa namna hiyo. “Lakini kwa hakika lazima tuchukue hatua yoyote ambayo inaweza kusaidia kwanza kusitisha mapigano, na kumaliza mzozo huu wa muda mrefu, na kufikia azimio kulingana na suluhisho la serikali mbili”.
Kardinali Parolin anatarajia kuwa na mkutano Jumamosi ijayo ambapo ni kati ya Papa na rais wa Tume ya Ulaya, Bi Ursula von der Leyen, ambaye pia kama Katibu wa Vativan atapata fursa ya kukutana naye. Kardinali amesema itakuwa fursa mpya kujadili mgogoro huo: “Kiukweli nitazungumza naye juu ya suala la Israeli na Palestina. Tutalazimika kuunganisha pamoja guvu ili kutafuta kumaliza mgogoro huu”.