Siri za majumba ya makumbusho Vatican zaanza kuoneshwa kwenye safu za video!

Safu za video za kuonesha Siri za Majumba ya Makumbusho Vatican zimeanza kuoneshwa tangu tarehe 20 Aprili kwa ushirikiano kati ya Majumba ya Makumbusho Vatican na Radio Vatican ili kuweza kujua siri zake za mkusanyo huo mzuri wa kipapa.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican.

Siri na  historia zisizojulikana, udadisi huliofichika nyuma ya uzuri unaotambulika ulimwenguni wa kazi bora za makusanyo ya Vatican. Celata Pulchritudo.( calata pulkritudo ), Siri za Makumbusho ya Vatican”, ni mpango  mpya wa vyombo vya habari ulioundwa kwa ushirikiano kati ya Radio Vatican  na Makumbusho ya Vatican. Kuanzia tarehe 20 Aprili 2021  safu ya video fupi zimeanza kutolewa zikikusudia kuelezea sanaa ya makusanyo ya kipapa kwa njia mpya.

Kutoka katika vyanzo vya msukumo wa walimu wakubwa kama vile Michelangelo au Raphaeli, hadi haiba na siri ya ustaarabu wa zamani kabla ya Ukristo; kutoka nyuma ya pazia la Jumba la makumbusho limezingatiwa na vizazi vya wasanii kuwa shule ya ulimwengu, kwa urithi wa maarifa, utafiti, uhifadhi na urejeshwaji na kuorodhwa hadi kufikia sisi kupitia karne zote.

Mchakato wa kusimulia hayo utaendelezwa kila mwezi kwa mwaka mzima kupitia matoleo mawili ya video: moja iliyo na maelezo ikiambatana na nakala ya maelezo, nyingine fupi inayolenga hadhira ya mitandao wa kijamii. Yaliyomo yatasambazwa kupitia tovuti na mtandao wa kijamii wa Vatican News na Makumbusho ya Vatican.

SIRI ZA MAJUMBA YA MAKUMBUSHO

Itakuwa njia ya kutoa mwonekano mpya kwenye Makumbusho ya Vatican ambayo, yalifungwa katika miezi ya hivi karibuni kufuata kanuni za sasa juu ya janga la Covid-19, hata hivyo hawajawahi kuacha, kwa kujibu wito wao kama mahali pa kuishi. “Celata Pulchritudo” pia ni fursa ya kujifunza juu ya wataalamu na ujuzi tofauti ambao kila siku hujiweka katika huduma ya taasisi iliyoundwa kudhihirisha uzuri kwa ulimwengu, na kwa maana nyingine  ni njia ya upendeleo ya kukutana na Mungu.

Hata kazi zinazojulikana zaidi na zilizopigwa picha zaidi kwa mujibu wa  Andrea Tornielli, mkurugenzi wa wahariri wa vyombo vya habari, Vatican  amesema kuna habari ambazo hazijulikani na ambazo zinahitaji udadisi na mambo ya kugundua: shukrani kwa msaada wa wale wanaojifunza, kutunza, kurejesha na kuhifadhi, jaribu hili linafanikiwa ili  kuwaleta karibu watu wengi iwezekanavyo katika hazina hizi za uzuri.

Jumba la makumbusho kwa hakika hasa watu wote kwa mujibu wa maoni ya Monsinyo Paolo Nicolini naibu mkurugenzi wa majumba ya Makumbusho ya Vatican  amesema ni wanawake na wanaume wanaofanya kazi kila siku kuhifadhi na kukuza moja ya makusanyo maarufu ya kazi bora ulimwenguni. Ni kwao hao  wahusika wakuu wa mpango huu, ambao  shukrani zake zinawaendea

21 April 2021, 16:32