Sherehe za Pasaka:Leo tunasheherekea tukio la matumaini!

Katika Misa ya Papa Francisko Jumapili tarehe 4 Machi 2021 katika ibada ya Ufufuko wa Bwana,mara baada ya Injili kumekuwa na ukimya wa tafakari bila mahubiri.Video fupi inaonesha baadhi ya matukio yaliyojionesha wakati wa Misa hiyo.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican.

Papa Francisko ameongoza Misa Takatifu ya Pasaka, Jumapili asubuhi tarehe 4 Aprili 2021, katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro mahali ambapo mara baada ya Injili ametoa muda wa ukimya wa tafakari ya kina. Na baada ya misa Takatifu Papa Francisko ametoa ujumbe wa Pasaka wa “Urbi et Orbi” kwa ajili ya mji na ulimwengu mzima huku akisisitiza jinsi ambavyo leo hii tunasherehekea tukio ambalolinatupatia tumaini ambalo halitukatishi tamaa. “Yesu aliyesulubiwa amefufuka”. Video fupi inaonesha tukio lililokuwa linatendeka leo hii katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, licha ya vizuizi vilivyopo vya janga la sasa la ulimwengu.

04 April 2021, 15:32