Mkutano mjini Vatican kuhusu itikadi kali za kidini
VATICAN NEWS
Baraza la Kipapa kwa ajili ya Mazungumzo ya kidini tarehe 26 na 27 Januari wamekuwa na mkutano kwa njia ya mtandao na siyo kwa umma kwa kuongozwa na mada: “Itikadi kali za kidini. tafsiri na Majibu ya wakristo na waislamu. Katika mkutano huo walishiriki wataalam na viongozi wa masuala ya dini za kikristo na za kiislamu.
Katika mchakato wa mkutano huo wametathimini matukio mbali mbali ya itikadi kali za kidini na vurugu, kusoma mizizi yake, njia za kueneza, pamoja na juhudi na mipango iliyopitishwa ili kukomesha na kuzuia mchakato huu. Mkutano unajikita katika kazi ya kudumu ya baadhi ya Ofisi za Vatican kwa ajili ya kuelewa hali hii ya kushangaza na kushirikiana katika kuhamasisha na kukuza utamaduni wa mazungumzo na udugu.
Katika maandalizi hayo wamchangia Ofisi ya Katibu wa Vatican, Baraza la Kipapa la Uinjilishaji wa Watu, Baraza la Kipapa la Elimu Katoliki, Baraza la Kipapa la Kahamasisha Maendeleo Fungamani ya Binadamu na Taasisi ya Kipapa ya Mafunzo ya Kiarabu na Kiislamu.