Majumba ya makumbusha yanafunguliwa Mosi Februari
katika taarifa iliyotolewa kupitia Instagram inasema kuwa kuanzia Mosi Februari,majumba ya makumbusho yanafunguliwa. kwa mara nyingine milango yake ili kutembelewa kama ilivyokuwa tayari imekwisha taarifiwa.
Na Sr. Angela Rwezaula - Vatican.
Kuanzia Jumatatu tarehe Mosi Februari2021, japokuwa ni ngumu. Kwa kupitia Instagram ya mkusanyo wa picha za Kipapa, imethibitishwa habari hiyo ambayo ilikuwa tayari imetolewa tarehe 14 Januari na Mkurugenzi wake Bi Barbara Jatta akizungumza na Vatican News.
Baada ya siku 88
Kwa mujibu wa habari iliyotolewa jioni tarehe 29 Januari 2021, inasema kuwa baada ya siku 88 za kufungwa, kuanzia tarehe Mosi Februari Majumba ya makumbushao yatafunguliwa kwa mara nyingine tena ili kuwezesha kurudi kutembelea majumba hayo kila siku kuanzia Jumatatu hadi Jumamosi saa 2.30 asubuhi hadi saa 12.30 jioni, kuingia mwisho ni saa 10.30 jioni. Ili kuweza kuingia lazima kuomba kupitia kwenye Tovuti ya Majumba ya Makumbusho Vatican
30 January 2021, 13:15