MOSI FEBRUARI FUNGUZI KWA MARA NYINGINE TENA WA MAJUMBA YA MAKUMBUSHAO VATICAN. MOSI FEBRUARI FUNGUZI KWA MARA NYINGINE TENA WA MAJUMBA YA MAKUMBUSHAO VATICAN. 

Majumba ya makumbusha yanafunguliwa Mosi Februari

katika taarifa iliyotolewa kupitia Instagram inasema kuwa kuanzia Mosi Februari,majumba ya makumbusho yanafunguliwa. kwa mara nyingine milango yake ili kutembelewa kama ilivyokuwa tayari imekwisha taarifiwa.

Na Sr. Angela Rwezaula - Vatican.

Kuanzia Jumatatu tarehe Mosi Februari2021, japokuwa ni ngumu. Kwa kupitia Instagram ya mkusanyo wa picha za Kipapa, imethibitishwa habari hiyo ambayo ilikuwa tayari imetolewa tarehe 14 Januari na Mkurugenzi wake Bi Barbara Jatta akizungumza na Vatican News.

Baada ya siku 88

Kwa mujibu wa habari iliyotolewa jioni tarehe 29 Januari 2021, inasema kuwa baada ya siku 88 za kufungwa, kuanzia tarehe Mosi Februari Majumba  ya makumbushao yatafunguliwa kwa mara nyingine tena ili kuwezesha kurudi kutembelea majumba hayo kila siku kuanzia Jumatatu hadi Jumamosi saa 2.30 asubuhi hadi saa 12.30 jioni, kuingia mwisho ni saa 10.30 jioni. Ili kuweza kuingia lazima kuomba kupitia kwenye Tovuti ya Majumba ya Makumbusho Vatican

UFUNGUZI WA MAJUMBA YA MAKUMBUSHO TAREHE 1 FEBRUARI
30 January 2021, 13:15