Kutokana na Covid,inabadilisha ibada ya majivu
Na Sr. Angela Rwezaula, - VATICAN NEWS
Hali halisi ya kiafya inayosababishwa na ugonjwa wa virusi vya corona unaendelea kuhitaji mfululizo wa tahadhari ambazo pia zinaoneshwa katika muktadha wa liturujia. Kwa kuzingatia hayo katika mwanzo wa Kwaresima mwaka huu, Baraza la Kipapa la Ibada na nidhamu ya Sakramenti imejulisha kupitia Tovuti yake maelekezo ambayo yanatakiwa washereheshaji wazingatie katika ibada ya kuweka majivu ambayo itakuwa ni Jumatano tarehe 17 Februari 2021.
Baada ya kubariki majivu na kuyanyunyizia kwa maji matakatifu, kwa mijibu wa taarifa hiyo, kuhani atawageukia washiriki waliopo huku akisoma mara moja maandiko yote kama ilivyo katika Misale ya Roma: “Badilika na kuamini Injili”, au “Kumbuka, mwanadamu, wewe ni mavumbi na utarudi mavumbini”.
Katika taarifa hiyo aidha inabainisha kuwa “kuhani atasafisha mikono yake na atavaa barakoa ili kulinda pua na mdomo wake, baadaye anawapaka majivu wale watakao mkaribia au, ikiwa inafaa, yeye mwenyewe atakwenda kwa wale wote ambao watakuwa wamesimama katika nafasi zao”. Kuhani, atahitimisha kwa kuchukua majivu na kuwapaka kichwa, bila kusema chochote.