2020.06.25 Rais wa  IFAD Gilbert Hounbo 2020.06.25 Rais wa IFAD Gilbert Hounbo 

Vatican yatoa msaada wa dhati kwa Ifad ili kupambana na njaa

Kwa mujibu wa Gazeti la kila siku la ‘Osservatore Romano’ limetoa taarifa juu ya maamuzi ya Vatican katika kutoa msaada muhimu kwa Shirika Umoja wa Mataifa la Mpango na Chakula (IFAD) ambalo kwa ahika liko katika shughuli ya kuwa karibu sana na maskini. “Jumuiya ya kimataifa lazima iunganishe nguvu kwa ajili ya uendelevu wa wakati ujao na haki kwa wote”,kwa mujibu wa Kardinali Pietro Parolin,Katibu wa Vatican.

Kwa upande wa Shirika la Mpango na Chakula IFAD linatoa shukrani na maelezo  kwamba msaada wa dola za kimarekani 25,000 ambazo zimetolewa na Vatican zinaweza kusaidia na kuendeleza shughuli za Shirika la Umoja wa Mataifa ambalo linajikita katika mapambano dhidi ya njaa na umaskini ulimwenguni kote.

Jumuiya kimataifa iunganishe nguvu zake

Kwa mujibu wa  Gazeti la Osservatore Romano,  hata hivyo linaonesha jinsi ambavyo katika tovuti ya IFAD, imetaja barua ya Kardinali Parolin kwamba anasisitiza umuhimu wa kuanzisha jambo hili. “Haiwezekani kwa urahisi tu kubaki kimya mbele ya mateso mengi haya namna hii. Leo hii kuliko hapo awali, Jumuiya ya kimataifa lazima iunganishe nguvu zake ili kuwandaa na kutimiza wakati ujao ambao uwe endelevu, jumuishi na wenye  haki kwa wote. Haya ndiyo tunapaswa kufanya na ndiyo wajibu wetu wa kusaidia watu walio maskini zaidi na waathirika katika ulimwengu huu”. Kwa mujibu wa Kardinali katika barua yake.

Umuhimu wa kufanya kazi pamoja

Tangazo la mchango wa Vatican limetolewa tarehe 11 Desmba katika mutadha wa mchakato mpya wa hukusanyaji wa fedha kwa ajili ya IFAD kwa upandw wa Nchi wanachama. Kwa mtzamo huo, Rais wa IFAD, Bwana Gilbert F. Houngbo, amesea kuwa “ni muhimu kufanya kazi pamoja kwa ajili ya kubadili mifumo yetu ya chakula na kuongeza matarajio na ustawi wa watu wa vijijini ambao wanamazingira magumu zaidi ulimwenguni”.

12 December 2020, 18:30