Tafuta

C9  Baraza la Makardinali washauri wa Papa C9 Baraza la Makardinali washauri wa Papa 

Baraza la Makardinali washauri wa Papa wafanya mkutano Desemba Mosi!

Kwa mujibu wa taarifa za vyombo vya habari, limethibitisha kuwa Baraza la Makardiali washauri wa Papa wamefanya mkutano wao tarehe 1 Desemba 2020 kwa ya mtandao.

VATICAN NEWS

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa msemaji wa vyombo vya habari  Vatican amethibitisha juu ya kufanyika mkutano wa Baraza la Makardinali washauri wa Papa  tarehe 1 Desemba 2020, jioni saa 10:00. Katika muktadha wa sasa wa janga la kiafya, mkutano huo umefanyika kwa njia ya mtandao. Waliounganishwa kwenye mkutano huo ni Kardinali Óscar A. Rodríguez Maradiaga, S.D.B., Kardinali Reinhard Marx, Sean Patrick O’Malley, O.F.M. Kap., Kardinali Oswald Gracias, na Kardinali Fridolin Ambongo Besungu, O.F.M. Kap., wakati mjini Vatican walikuwepo Kardinali Pietro Parolin, Kardinali Giuseppe Bertello na Katibu wa Baraza la makardinali washauri, Askofu Marco Mellino.

Hata  na Papa Francisko ameshiriki mkutano huo kwa  kuunganishwa akiwa katika Makazi yake nyumba ya Mtakatifu Marta. Baada ya salam fupi, Papa Francisko amewakilisha kwa washiriki wa mkutano huo, mjumbe mpya wa Baraza hilo la ushauri ambaye ni Kardinali Ambongo Besungu, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu katoliki la Kinshasa na baadaye wakaendelea kutoa baadhi ya michango ya mawazo kuhusiana na maisha ya Kanisa katika mabara tofauti, kwa namna ya pekee wakitazama hali halisi iliyopo ya kiafya.

Katibu wa Baraza la makardinali washauri wa Papa, ameweza  kusoma kwa ufupi yatokanayo, katika hatua za mchakato wa Mswada mpya wa Katiba ya kitume  na wakati huo huo uchunguzi, marekebisho na mapendekezo yaliyopokelewa kutoka Mabaraza ya kipapa yalishughulikiwa katika miezi ya hivi karibuni. Mkutano unaofuata umependekezwa kufanyika mwezi wa Februari 2021.

02 December 2020, 12:53