Asubuhi ya Papa katika maombi ya kuombea Roma na ulimwengu

Alfajiri na mapema sana, Papa Francisko amekwenda katika sanamu ya Bikira Maria iliyoko katikati ya mji wa Roma kwa ajili ya kuto heshima ya faragha kwa Bikira Maria.Kabla ya kurudi Vatican amepitia Kanisa kuu la Mtakatifu Maria Mkuu mahali ambapo amesali mbele ya picha ya Maria Salus Popoli Roman na kuadhimisha Misa katika Kikanisa cha Mtakatifu Yosefu.

Tarehe 8 Desemba 2020 ni siku ambayo Mama Kanisa anaadhimisha Siku Kuu ya Bikira Maria Mkingiwa dhambi ya Asili. Katika mwanga wa mapambazuko ya siku na ukimya ya mji wa Roma kutokana na mvua iliyokuwa ikinyesha, Papa Francisko amefika saa 1:00 kamili asubuhi katika Uwanja wa Hispania kwa ajili ya tendo la kutoa heshima kwa Bikira Maria mkingiwa wa dhambi ya Asili. Chini ya miguu ya Sanamu ya  Maria, Papa amesali huku  akielekeza macho juu ya Mama wa Mungu. Baadaye ameweka shada la maua ya mawiridi meupe.

Maombi ya Papa

Maombia hayakusindikizwa kama ilivyo kiutamaduni katika fursa  kama hiyo yaani kwa kawaida kuzungukwa na umati mkubwa wa watu, kwa maana katika siku hii, Papa amekwenda katika muda ambao siyo wa kawaida katika uwanja wa Hispania, yaani asubuhi na siyo mchana kwa sababu ya hali halisi ya kiafya ili  kuzuia hatari la mkusanyiko wa watu wengi ambao wanaweza kusababisha maambukizi, kama walivyokuwa tayari wameshatoa taarifa.

Sala ya Papa

Kwa mujibu wa msemaji wa vyombo vya habari Vatican, Papa amemkabidhi Mama Maria watu  wote ambao katika mji huu na katika ulimwengu wanasumbuliwa na ugonjwa na kukata tamaa. Kabla ya saa 7:15, asubuhi, Papa Francisko ameacha uwanja huo wa Hispania na kuelekea katika Kanisa Kuu la Bikira Maria Mkuu na kusali mbele ya Picha ya Maria Salus Popoli Romani  na ameadhimisha Misa katika Kikanisa cha Mtakatifu Yosefu na baadaye kurudi mjini Vatican.

Misa ya Papa katika kikanisa cha Mtakatifu Yosefu
Misa ya Papa katika kikanisa cha Mtakatifu Yosefu
08 December 2020, 16:06