Wasifu wa makardinali wapya kutoka kona za ulimwengu!
Na Sr. Angela Rwezaula-Vatican.
Wafuatao ni wasifu wa makardinali wateule: Kardinali Mteule Mario Grech Katibu Mkuu wa Sinodi ya Maaskofu, alizaliwa huko Qala (Malta), jimbo la Gozo, tarehe 20 Februari 1957. Majiundo yake msingi na sekondari huko Victoria, Gozo; ikiwa ni pamoja na falsafa na taalimungu katika seminari ya Gozo. Baadaye aliendelea na Masomo ya juu katika Chuo kikuu cha kipapa la Laterano na pia kwa kujipatia udaktari wa Sheria za Kanisa katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Antony Aquine (Angelicum). Tarehe 26 Novemba 211 Papa Mstaafu Benedikto XVI akamteua kuwa Askofu wa Gozo, hadi tarehe 2 Oktoba 2019 alipotangazwa na Papa kuwa Katibu Mkuu mwandamizi wa Sinodi ya Maaskofu. Tarehe 5 Septemba 2020 akateuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Sinodi ya Maaskofu.
Kardinali Mteule Marcello Semeraro Rais wa Baraza la Kipapa la mchakato wa kuwatangaza Watakatifu, alizaliwa huko Monteroni ya Lecce Italia, tarehe 22 Desemba 1947. Akapata daraja la Upadre tarehe 8 Septemba 1971. Majiundo yake ya kikuhani ni kuanzia Seminari ya Kipapa ya Kikanda ya Pio XI huko Molfetta, Puglia. Na baadaye aliendelea na mafunzo katika kitivo cha taalimungu cha Chuo Kikuu cha Kipapa Laterano, Roma mahali alipopata shahada ya udaktari wa Taalimungu Takatifu. Aliendelea na kufundisha taalimungu katika Taasisi ya kanda ya Puglia, hata masomo ya Kikanisa katika Kitivo cha taalingumu cha P.U.L. Alichaguliwa kuwa Askofu tarehe 25 Julai 1998 na kuamishwa katika Kanisa la Jimbo la Albano kunako tarehe 1 Oktoba 2004 hadi tarehe 15 Oktoba 2020 alipoteuliwa na Papa Francisko kuwa Rais wa Baraza la Kipapa la Mchakato wa kuwatangaza watakatifu.
Askofu Mkuu Antoine Kambanda wa jimbo kuu katoliki Kigali (Ruanda,alizaliwa tarehe 10 Novemba1958 jimbo kuu Kigali. Kwa bahati mbaya ndugu zake wa familia waliuwawa wakati mauaji ya kimbari 1994 na akabaki na kaka yake ambaye kwa sasa anaishi Italia. Masomo yake ya msingi alisomea Burundi na Uganda, na kuhitimisha baadaye sekondari nchini Kenya. Alirudi nchini Rwanda akiwa amehitimisha masomo ya Falsafa na Taalimungu Mungu kwa miaka miwili. Alipata daraja la upadre kunako tarehe 8 Desemba 1990 mikononi mwa Mtakatifu Yohane Pauli II wakati wa ziara yake ya kichungaji nchini Rwanda. Baada ya daraja alishughulika na masuala ya seminario kama Gombera na kufundisha masomo katika seminari ya ndogo ya Ndera Kigali. Alendelea na Mafunzo ya juu katika Taasisi ya Alfonsiana, Roma, na kupata shahada ya udaktari wa Taalimungu maadili. Aliporudi Rwanda akawa Mkurugenzi wa Caritas Jimbo kuu Kigali na Tume ya Jimbo kwa ajili ya Haki na amani. Profesa wa Taalimungu maadili katika seminari kuu ya taalimungu Nyakibanda. Kunako tarehe 7 Mei 2013 aliteuliwa kuwa Askofu wa Jimbo la Kibungo hadi tarehe 19 Novemba 2018 ambapo Papa Francisko alimetua kuwa Askofu Mkuu wa jimbo Kuu Kigali.
Kardinali Mteule, Askofu Mkuu Wilton D. Gregory wa Washington. Alizaliwa tarehe 7 Desemba 1947 huko Chicago (Illinois) Marekani. Baada ya shule ya msingi na huko Chicago, alijiunga na Seminari ya maandalizi ya Quigley. Masomo ya kifalsafa huko taasisi ya Niles na baadaye taalimungu katika Seminari ya Mtakatifu Maria huko Mundelein (Illinois) Marekani. Aliendelea na masomo ya juu na kupata shahada ya Udaktari wa Liturujia Katika Taasisi ya Mtakatifu Anselmi Roma(1980). Alipata daraja la Upadre tarehe 9 Mei 1973 jimbo kuu katoliki la Chicago. Baada ya upadrisho akashika nyadhifa mbali mbali za jimbo. Na baadaye akarudi tena kuwa mwanafunzi Roma (1976-1979). Aliteuliwa kuwa Askofu Mkuu msaidizi wa Atlanta (Georgia) kunako tarehe 4 Desemba 2004. Amewahi kuwa Rais wa Baraza la Maaskofu Marekani (2001-2004). Tarehe 4 Aprili 2019 aliteuliwa na Papa Francisko kuwa Askofu Mkuu wa Washington.
Kardinali Mteule, Askofu Mkuu Jose F. Advincula wa Capiz (Ufilippine). Alizaliwa huko Dumalag, Jimbo Kuu katoliki la Capiz, tarehe 30 Machi 1952. Baada ya masomo yake ya msingi huko Dumalag, aliendelea na seminari ya Mtakatifu Pius X mji wa Roxas mahali ambapo aliendelea hata na masomo ya kifalsafa, na baadaye Taalimungu katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Tomas huko Manila. Alipata daraja la upadre jimbo Kuu la Capiz tarehe 14 Aprili 1976. Baada ya daraja alishika nafasi mbali za Kanisa lakini baadaye akaendelea na Mafunzo tena katika Chuo Kiuu cha Mtakatifu Tomas Angelicum, Roma kwa kupata Uzamifu wa Sheria za Kanisa. Amekuwa mhamasishaji wa Haki na amani katika Mahakama ya Jimbo Kuu la Capiz. Aliteuliwa kuwa Askofu kunako tarehe 15 Julai 2001 kuwa Askofu wa Mtakatifu Carlos, na kusimikwa tarehe 8 Septemba mwaka huo. Tarehe 9 Novemba 2011 aichaguliwa kuwa Askofu Mkuu wa Capiz, katika kisiwa cha Panay, Ufilippine ya Kati .
Kardinali mteule, Askofu mkuu Celestino Aós Braco, o.f.m. kap wa Santiago ya Chile. Alizaliwa Artaiz, Jimbo Kuu la Pamplona (Uhipagna), tarehe 6 Aprili 1945. Majiundo yake ya kifalsafa huko Zaragoza na taalimungu Pamplona. Amepata uzamili wa masomo ya saikolijia chuo Kikuu cha Barcellona (Uhispagna). Alifunga nadhiri za muda katika Shirika la Ndugu wadogo wakapuchini, tarehe 15 Agosti 1964 huko Sangüesa na za milele tarehe 16 Septemba 1967 huko Pamplona. Alipata daraja la Upadre huko Pamplona tarehe 30 Machi 1968. Alichaguliwa kuwa Askofu wa Copiapó, tarehe 25 Julai 2014, na kuwekwa wakfu tarehe 18 Oktoba mwaka huo huo. Tarehe 23 Machi 2019 aliteuliwa kuwa Msimamizi wa Kitume katika jimbo kuu lisilo na Askofu la Santiago ya Chile. Tarehe 27 Desemba 2019 Papa Francisko amteua kuwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Santiago ya Chile.
Kardinali mteule, Askofu Cornelius Sim wa Puzia ya Numidia na Msimamizi wa Kitume wa Brunei. Alizaliwa huko Seria (Brunei) tarehe 16 Septemba 1951. Majiundo ni kuwa na shahada ya uhandisi kutoka Chuo Kikuu cha Dundee, Scotland, Uingereza. Ana Shahada ya Uzamili katika Taalimungu kutoka Chuo Kikuu cha kifranciskani cha Steubenville, Ohio, Marekani. Alipata daraja la Upadre tarehe 26 Novemba 1989. Baada ya kufanya shughuli za uchungaji wa parokia, alitangazwa kunako mwaka 1995 kuwa Msimamizi mkuu wa Brunei na tarehe 21 Novemba 1997 akateuliwa Kuwa balozi. Mnamo tarehe 20 Oktoba 2004, Mtakatifu Yohane Paulo II aliinua Jimbo la Kitume la Brunei na kumteua kuwa Msimamizi wa kwanza wa Kitume,na kuwa na makao ya uaskofu wa Puzia ya Numidia.
Kardinali mteule, Askofu Mkuu Augusto Paolo Lojudice wa Siena-Colle Val ya Elsa-Montalcino, Italia. Alizaliwa Roma tarehe 1 Julai 1964. Baada ya masomo yake ya mwanzo alijiandaa na mafunzo ya kikuhani katika Seminari Kuu ya Kipapa ya Roma na kuendelea na masomo ya Falsafa na Taalimungu katika Chuo Kikuu cha Kipaap cha Gregoriana, tangu 1983 hadi 1988. Alipata shahada ya Taalimungu Msingi. Alipewa daraja la Upadre tarehe 6 Mei 1989, Jimboni Roma. Baada ya upadirisho alishika nafasi mbali bali za utume. Tarehe 6 Machi 2015 alichaguliwa kuwa Askofu kwa ajili yaAlba ya Marittima na Msaidizi Roma. Aliwekwa wakfu wa kiasfu tarehe 23 Mei mwaka huo huo. Ni katibu wa Tume ya Baraza la Maskofu Italia (CEI) kitengo cha wahamiaji. Tarehe 6 Mei 2019 Papa Francisko alimteua kuwa Asofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Siena-Colle Val ya Elsa-Montalcino.
Fr. Mauro Gambetti, o.f.m. Konv. Msimamizi wa Comvti Takatifu ya Assisi. Alizaliwa tarehe 27 Oktoba 1965 huko Castel san Pietro Terme (Bologna). Baada ya shahaha ua uandisu wa ufundi chuo kikuu cha Bologna kunako mwaka 1992 alianza rasmi safari ya kiroho katika shirika wa Ndugu wadogu wa Wakomventuali ambao baada yam waka mmoja wa unovisi aliweka nadhiri zake za muda kunako tarehe 29 Agosti 1995 na za milelel tarehe 20 Septemba 1998. Aliendelea na Masomo yake usaktari wa Taalimungu Taasisi ya Kitaalimungu Assisi. Baada ya mafunzo ya Taalimungu katika Taasisi ya Kitaalimungu ya Assisi (Perugia), alipata shahada ya uzamili katika Taalimunu ya mtu katika Kitivo cha kitaalimungu cha Italia ya Kati huko Florence. Alipewa daraja la upadre kunako tarehe 8 Januari 2000 huko Longiano(Forlì-Cesena) mahali ambapo, katika conventi ya watawa wa Msalaba Mtakatifu alishikilia wadhifa wa uhuishaji wa huduma ya vijana na wito kwa mkoa Emilia-Romagna na, kutoka 2005 hadi 2009, wa kuongoza jumuiya ya kidini. Tangu 2013 hadi uteuzi alikuwa anaendelea kuwa msimamizi wa Conveti takatifu ya Assisi. Mara baada ya kupata habari hizo, Fra Mauro amesema “ haya ni matani ya Papa na kwamba anapokea kwa utambuiz na furaha habari hii kwa roho ya utii wa Kanisa na huduma ya ubinadamu katika wakati huu mgumu kwa wote. Amemkabidhi Mtakatifu Francis safari yake na kufanya maneno yake ya udugu kuwa ya kwake.
Kardinali Mteule, Askofu mstaafu Felipe Arizmendi Esquivel wa Mtakatifu Cristobal de las Casas, alizaliwa tarehe1 Mei 1940 huko Chiltepec, manispaa ya Coatepec Harinas (serikali ya a Mexico, wakati huo ilikuwa ndani ya jimbo kuu la Mexico na leo ni jimbo la Toluca). Alikamilisha masomo yake ya ubinadamu na falsafa katika seminari ya Toluca na ile ya taalimungu katika Chuo Kikuu cha Kipapa cha Salamanca (Uhispania),ambapo alipata uzamili wa katika Taalimungu akaendelea na mfunzo zaidi ya y Liturujia. Alipata daraja la upadre tarehe 25 Agosti 1963 huko Toluca, na kupewa majukumu mengi. Mnamo tarehe 7 Februari 1991 aliteuliwa kuwa askofu wa Tapachula na aliwekwa wakfu kwa kiaskofu tarehe 7 Machi mwaka huo huo. Katika kipindi hicho alikuwa Katibu Mkuu wa CELAM. Mnamo tarehe 30 Machi 2000, Mtakatifu Yohane Paulo II alimteua kuwa Askofu wa San Cristóbal ya Las Casas hadi tarehe 3 Novemba 2017.
Kardinali mteule, Askofu Mkuu Silvano M. Tomasi, Askofu wa Asolo, na Balozi wa Kitume, alizaliwa tarehe 12 Okotba 1940 huko Casoni ya Mussolente (Italia). Alipata mafunzo ya kielimu nchini Italia na Marekani ambapo alisomea taalimungu na akapewa daraja la upafre tarehe 31 Mei 1965 katika Shirika lwa Wamishonari wa Mtakatifu Caroli la Wascabrini.NAnayo Shahada ya Sayansi ya Jamii na Udaktari katika Elimu ya Jamii kutoka Chuo Kikuu cha Fordham huko New York Marekani. Kuanzia mwisho wa 1989 hadi Juni 1996 alikuwa Katibu wa Baraza la Kipapa la Huduma ya Kichungaji kwa ajili ya Wahamiaji na Watu Wanaosafiri. Mnamo tarehe 27 Juni 1996 aliteuliwa kuwa askofu mkuu wa Cercinia na Balozi wa kitume nchini Ethiopia, Eritrea na mwakilishi katika Umoja wa Afrika. Mnamo tarehe 24 Aprili 1999 aliteuliwa kuwa Askofu Mkuu wa Asolo na tarehe 23 Desemba 2000 aliteuliwa kuwa Balozi wa kitume huko Giubuti. Mnamo tarehe 10 Juni 2003 aliteuliwa kuwa mwakilisho wa Kudumu wa Vatican katika Ofisi za Umoja wa Mataifa na Taasisi Maalum huko Geneva na Mwakilisho wa Kudumu katika Shirika la Biashara Ulimwenguni (O.M.C.). shughuli iliyofanyika hadi tarehe 13 Februari 2016. Tarehe 9 Aprili 2026 Papa Francisko alimteua kuwa mjumbe tayari wa Baraza la kiapa la Haki na amano leo hii ni Baraza la Huduma ya Maendeleo Fungamani ya watu.
Kardinali mteule, Padre Raniero Cantalamessa (o.f.m. kap), mhubiri wa Nyumba ya Kipapa. Alizaliwa huko Colli ya Tronto (AP) Italia, kunako tarehe 22 Julai 1934. Alipewa daraja la upadre kunako 1958. Msomo yake ya kitaalimungu hulo Friburg, Uswiss, pia katika masomo ya Fasihi Asili katika Chuo Kikuu Katoliki cha Milano. Amekuwa profesa kamili wa Historia ya asili ya Kikristo na Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi ya Dini ya Chuo Kikuu cha Moyo Mtakatifu huko Milano. Amekuwa mjumbe wa Tume ya Kimataifa ya taalimungu tangu mwaka 1979 akaacha kufundisha na kujikita katika huduma ya kutangaza Neno. Ni Mfansiskani Mkapuchini ambaye tarehe 23 Juni 1980, Mtakatifu Yohane Paulo II alimteua kama mhubiri mkuu katika nyumba ya kipapa kwa kutoa tafakari na sala katika vipindi vikuu vya kiliturujia kama vile Majilio na Kwaresima kwa ushiriki wa mapapa wote watatu, kuanzia Yohane Paulo II, Benedikto XVI na sasa Papa Francisko, na Sekretarieti nzima ya Roma. Kwa maana hiyo nafasi hiyo imeweza kuthibitishwa kuanzia na Mtakatifu Yohane Paulo II kunako mwaka 2005 na Ratzinger, Papa Mstaafu Benedikto XVI na kunako 2013 na (Bergoglio) Papa Francisko.
Kardinali Mteulie, Padre Enrico Feroci, Paroko wa Mtakatifu Maria wa Upendo wa Mungu huko Castel ya Leva. Alizaliwa tarehe 27 Agosti 1940 huko Pizzoli. Alijiunga na Seminari ndogo ya kipapa akiwa na miaka 11 na baada ya masomo akaendelea na Seminari kuu. Alipewa daraja la upadre tarehe 13 Machi 1965. Ameshika nafasi mbalimbali katika utume wake. Ni mshauri wa Baraza la kipapa la Uchungaji kwa ajili ya wahamiaji na wakimbizi. Tarehe 10 Novemba 2017 Kardinali wa Roma alimteua kuwa rais wa chama cha Kilei cha Umma cha Watoto wa Mama wa Mungu upendo na kumpatia usimamizi wa Madhabahu ya Upendo wa Divino ( Madhabahu ya Mama Maria) pia ni Gombera wa Seminari ya Maria wa upendo wa Mungu tangu tarehe 1 Septemba 2018.