Papa Francisko katika mkutani na wajumbe wa Kamati ya Tuzo 'Zayed Award for Human Fraternity'' Papa Francisko katika mkutani na wajumbe wa Kamati ya Tuzo 'Zayed Award for Human Fraternity'' 

Papa Francisko akutana na tume kwa ajili ya tuzo ya Zayed ya Udugu wa ubinadamu!

Wajumbe wa Kamati ya Tuzo ya 'Zayed ya udugugu wa kibinadamu wako Roma ,kujadili sheria na vigezo vya tuzo na ambapo wamekutana na Papa.Chombo hiki kiliundwa mnamo 2019,kwa kutambuliwa na Papa Francisko na Imam Mkuu Ahmad al Tayyeb kwa kusaini Hati juu ya Udugu huko Abu Dhabi. Mwaka huu, kwa mara ya kwanza, tuzo hiyo inatoa fursa ya kuteua mtu maalum na taasisi ambazo zimetoa mchango mkubwa kwa ajili ya ubinadamu.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Tume ya  majaji wa kwa ajili ya  Tuzo ya Zayed ya Udugu wa ubinadamu wamekutana na Papa Francisko kwa mara ya kwanza tarehe 23 Oktoba 2020. Fursa  hiyo ilikuwa ni katika kikao cha kufanya kazi kilichopangwa huko Roma ili kujadili mifumo ya tathmini ambayo majaji  hao watafuata hadi kutangazwa kwa mshindi mnamo Januari 2021. Katika mchakato wa mkutano wao, wametoa fursa ya kuteua mtu maalum na taasisi ambazo zimetoa mchango mkubwa kwa ajili ya ubinadamu

Jumatatu, tarehe 19 Oktoba, (HCHF) chombo hiki kilitangaza wito wa maombi ya duru ya pili ya tuzo na ni kwa mara ya kwanza hii kutokea. Katika kikao cha ufunguzi, utambuzi huo uliwaendelea Imam Mkuu wa Al-Azhar, Al-Sharif, profesa., Ahmed Al-Tayyeb, na Na  Papa Francisko kutokana na  jukumu lao katika kusaini Hati juu ya Udugu wa Binadamu (DHF) huko Abu Dhabi, Februari 2019.

Wajumbe wa Tume hiyo ya kuandaa  Tuzo ya Zayed ya Udugu wa Binadamu waliipongeza Hati hiyo (DHF), wakionyesha umuhimu wake kwa wanadamu wote, hasa kwa kuzingatia changamoto na shida ambazo ulimwengu unapitia. Walitoa pongezi pia juhudi zilizofanywa na tuzo ya udugu wa kibinadamu (HCHF) kukuza utamaduni wa kuishi pamoja, na pia mpango wa kuunga mkono tuzo na kuweka vigezo katika tuzo yake. Tume hiyo ya majaji ilionyesha shukrani zao kwa utayari wa UAE kuunga mkono juhudi za kufikia malengo ya DHF.

24 October 2020, 11:07