Kard.Tagle:Wote tunaitwa kujua,kupenda na kutangaza Injili kwa kushuhudia!
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Katika Ujumbe wake kwa njia ya video katika fursa ya maadhimisho ya siku ya kimisionari ulimwenguni tarehe 18 Oktoba 2020, Kardinali Luis Antonio G. Tagle, Rais wa Baraza la Kipapa la Uinjilishaji wa Watu, na Rais wa Caritas Internationalis, amesema kuwa jitihada za umisionari kwa kila mbatizwa ni sehemu ya kujenga utambulisho wa kuwa mwamini kamili na kwa maana hiyo "wote tunaitwa kujua, kupenda na kutangaza Injili wakati tunashuhudia neno na matendo yetu ya dhati ya kutoa sadaka".
Akigusia kuhusu ujumbe wa Papa Francisko kwa ajili ya Siku ya Kimisionari 2020, Kardinali Tagle amebainisha kwamba “ Papa kwa njia ya Shirika la Kipapa la shughuli za kimisionari (PMS), anatoa msaada wake kiroho na zana kwa wamisionari hivyo wote tunapaswa kuhisi kuwa sehemu ya mchakato wa mwendelezo wa kimisionari kwa kushirikiana ili kuunga mkono kiuchumi katika utume wa kimisionari. Hata kama ulimwengu unapitiwa na changamoto za nguvu, lakini utume unaendelea na mahali pale ambapo kuna mahitaji zaidi, wapo pia wamisionari na ambao wanahitaji msaada wetu”, amehitimisha ujumbe wake kwa njia ya video Kardinali Tagle.