Maadhimisho ya Siku ya Kimisionari ulimwenguni ni tarehe 18 Oktoba 2020!
Katika kujibu baadhi maswali waliyoomba kujua juu ya maadhimisho ya Siku ya Kimisionari ulimwenguni kwa 2020, kwa mujibu wa Baraza la Kipapa la Uinjilishaji wa Watu, wanathibitisha kuwa maadhimisho hayo mwaka huu kwa ngazi ya ulimwengu, itafanyika siku ya Dominika tarehe 18 Oktoba, bila kuwa na mabadiliko yoyote katika kalenda. Kwa mujibu taarifa iliyotolewa aidha wanabainisha kuwa tayari majimbo mengi yamekwisha anza kwa muda maandalizi lakini bado inabaki uhamasishaji wa kimisionari kwa upande wa watu wa Mungu.
Imani ya kimisionari
Katika kuhitimisha taarifa yao wanasema imani, kiukweli, asili yake ni ya umisionari na maadhimisho ya Siku ya Kimisionari ulimwenguni kusaidia kubaki na mwelekeo huo muhimu wa imani ya Kikristo iliyo hai kwa waamini wote. Baraza la kipapa la Unjilishaji wa Watu aidha linakumbusha maana ya ushirikiano na uwajibikaji wa maaskofu na kusisitiza kwamba ukusanyaji wa sadaka kwa Siku hiyo ni kwa ajili ya Mashirika ya Kipapa ya Kimisionari,ambayo hufanya kazi katika muktadha huo wote wa ulimwengu kwa msaada ulio sawa wa Makanisa katika maeneo ya kimisionari.