Siku ya huduma za kibinadamu Ulimwenguni 2020:Kusaidia jumuiya mahalia!
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Kila tarehe 19 Agosti ya kila mwaka Umoja wa Mataifa unaadhimisha siku ya Kimataifa ya huduma za kibinadamu. Katika fursa hii Caritas internationalis inaangazia umakini kuhusu umuhimu wa jumuiya mahalia ili kuhakikisha yanatolewa majibu ya haraka katika muktadha wa msaada wa kibinadamu. Caritas intenationalis aidha inaomba utolewe msaada mkubwa kwa mashirika ya asasi za kiraia na hasa ya kidini kama vile Caritas ambayo inajikita kutoa msaada mkubwa sana na kuongeza nguvu za jumuiya katika maeneo mahalia.
Siku hii ya tarehe 19 Agosti ilitangazwa na Umoja wa Mataifa kunako mwaka 2008 kama kutoa jibu la shambulizi la kigaidi lililokuwa limetokea miaka mitano kabla, yaani kunako 2003 katika Mtaa ulio na Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa huko Baghdad, nchini Iraq na kusababisha vifo vya watu 22 miongoni mwao alikuwemo mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa nchini Iraq Sergio Vieira de Mello. Siku hii kwa hakika ni kutaka kuangazai zaidi ulinzi na usalama wa wafanyakazi wanaotoa huduma za kibinadamu sambamba na utu wao kwenye maeneo mengi yenye mizozo na kinzani ulimwenguni.
Mtu mmoja kati ya watu 45 ulimwenguni anahitaji msaada
Siku ya kimataifa ya huduma za kibinadamu aidha inawakumbuka wale wote ulimwenguni wanaofanya kazi katika maeneo magumu sana, yenye kuwa na majenga tofauti kama vile tememeko, vita, mafuriko na majanga mengine ya asili na yasiyo ya asili. Kwa mwaka huu 2020, siku hii inaadhimishwa katika muktadha wa janga la Covid-19 ambalo limeathiri na linaendelea kuleta matatizo makubwa na pia milipuko ambao umeangamiza jiji la Beirut nchini Lebanon. Katika wakati huu wa kihistoria Caritas internationalis inabainisha kuwa mfumo wa kibinadamu wa kimataifa umejaribiwa vikali sana kuliko hapo awali, na mtu mmoja katika kila watu 45 ulimwenguni anahitaji msaada. Katika siku hii jumuiya ya kimataifa inakumbuka ukarimu wa maelfu ya wahudumu wa kibinadamu, masikini na hasa walionusurika kwa majanga, wanaotamani kuishi kwa hadhi, kwa mujibu wa Aloysius John, katibu mkuu wa Caritas internationalis, ambaye anaonesha ukaribu wake kwa nchi zote ulimwengu .
Kutenga fedha kwa ajili ya mashirika ya asasi za kiraia
Caritas internationalis vile vile katika muktadha wa siku hii , inashauri serikali na jamuiya ya kibinadamu kimataifa kutenga fedha kwa kiwango kikubwa ili kuimarishaji asasi za kiraia na miundo yao msingi; kutenga fedha maalum kwa ajili ya uwezeshaji wa jamuiya za maeneo mahalia na kuiruhusu kuchukua hatua stahiki hasa inapotokea tukio la majanga. Caritas internationalis aidha inaomba kwamba serikali zote na jamuiya ya kibinadamu kimataifa zizingatie uwezeshaji wa mashirika ya asasi za kiraia, hasa mashirika ya kidini ambayo hufanya kazi sana karibu na watu wa jamuiya mahalia. Kwa maana hiyo ni muhimu kwamba mashirika haya yawe na rasilimali muhimu ili waweze kuandaa jamuiya mahalia katika kujibu kwa kujitegemea dharura zinapotokea.