Mei 29 itafanyika semina kupitia mtandao juu ya ulinzi wa watoto!
Mkutano wa Kimataifa wa Ulinzi na Usalama wa watoto (ISC), ambao kila mwaka hukusanya pamoja wawakilishi wa Kanisa, wataalamu na zaidi wataalam wa kisayansi juu ya mada ya ulinzi wa watoto ili kushirikishana maarifa na mazozi bora, umeandaa mfululizo mpya wa semina kupitia mtandaoni kuanzia tarehe 29 Mei 2020 ili kuweza kujadiliana pamoja, kwa kuongozwa na kauli mbiu Kanisa salama zaidi. Mfululizo wa semina hizo utazingatia njia ambazo wataalam wa kulinda wanajibu jumuiya, hasa kwa waathirika kwa kuimarisha mazoea mazuri ambayo tayari yamekomaa na inakusudia kuhamasisha Kanisa Katoliki na mashirika mengine ya kidini katika kutekeleza mipango yao ya ulinzi licha ya shida kubwa inayotarajiwa kufuatia na janga la Covid-19.
Wasiwasi kuhusu ulinzi wa watoto kufuatia na janga la uchumi
Kwa mujibu wa Padre Hans Zollner, Mhusika wa Kamati ya maandalizi ya Mkutano wa Kimataifa wa ulinzi na Usalama wa watoto (ISC), amebainisha kuwa kwa hakika kuna wasiwasi, kuhusu kupunguzwa kwa mipango ya kulinda watoto na watu wazima wanaoishi katika mazingira magumu, kufuatia mzozo na ugumu wa uchumi wa sasa. Kwa maana hiyo ameongeza kusema, “Hatuwezi kuruhusu uwekezaji wetu katika usalama wa watoto kwa njia sawa na shughuli zozote za kijamii na za kielimu”.
Kipeo cha kiafya na kipeo cha haki za watoto
Takwimu zilizoripotiwa na vyombo vya habari, katika nyakati za janga, zinaonyesha kuongezeka kwa ukatili dhidi ya watoto na kuongezeka kwa visa vya ukatili wa majumbani katika wiki za hivi karibuni. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa alisema kuwa shida ya kiafya iliyosababishwa na Covid-19 inageuka haraka kuwa shida ya haki za watoto, na wataalam wa lango la Ulinzi wa watoto wameelezea mashaka na wasiwasi juu ya watoto katika majumba hayo mbayo yangetakiwa kuwa mahali pa salama kwa ajili ya wote.
Mkutano wa kwanza kwa njia ya mtandao utafanyika tarehe 29 Mei 2020 saa 9:00 alasiri, ambapo kama walivyofahamisha Tume ya maandalizi ya mkutano kuhusu Ulinzi wa watoto, Kanisa ndiyo linachukua majukumu ya kulinda wakati wa kipindi hiki cha janga na kutilia maanani kwa namna ya kulinda waathiriwa.