Vatican yaongeza muda hadi Mei 3 katika hatua za kupambana na Covid-19
Hatua zilizopitishwa na Vatican, sanjari na hatua za serikali ya Italia za kuepusha kuenea kwa janga la Virusi vya Corona itaendelea hadi Mei 3. Uongezwaji wa muda huo umewasilishwa tarehe 14 Aprili 2020 katika Chumba cha Vyombo vya Habari Vatican kama ilivyo kawaida ya fursa nyingine.
Kwa nji hiyo shughuli za mamlaka ya Vatican zitaendelea, japokuwa kwa mahudhurio ya watu wachache ili kupunguza kwa kiasi fulani cha watu na kuhimiza kufanya kazi wakiwa mbali iwezekanavyo katika kupunguza mizunguko ya safari ya wafanyakazi na wakati huo huo kuwezesha uhakika wa huduma ya kharifa wa Mtume Petro kuendelea.
Hata hivyo kama ilivyokuwa imeanishwa katika hati ya Aprili 2, iliyosainiwa na Kardinali Pietro Parolin, Katibu wa Vatican ya kusimamishwa kwa shughuli za mahakama katika mji wa Vatican hadi Mei 4, mwanzoni ilikuwa imewekwa tarehe ya mwisho kuwa Aprili 3.