Caritas Internationalis:Wema na wepesi katika kusaidia walio hatarini!
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Watu wote matatizo mengi ambayo yamejionesha katika ulimwengu na ugonjwa wa virusi vya corona, lakini walio wengi hawana njia na zana sawa kuweza kupambana. Zaidi ya hayo siyo rahisi kuwaomba watu waheshimu kanuni za sheria zilizowekwa kufuatwa na jamii ikiwa wana njaa na hawajuhi ni wapi wanapate chakula. Au kuzingatia viwango vya afya ikiwa hakuna maji safi. Na ni katika pengo hili kwamba Caritas Internationalis inafanya kazi kwa kina, hata zaidi katika janga hili na zaidi ya yote kwa sababu Papa amewaomba wao moja kwa moja. Bwana Aloysius John amefafanua juu ya kwenda kukutana na Papa Francisko ili kumwakilishia matendo ya kazi baada ya covid-19 na akawambia kuwa, “Ninyi muwe wema na wepesi na kuendelea kupeleka mbele kazi yenu. Ikiwa hamfanyi ninyi, je ni nani atafanya hivyo”.
Baraza la kipapa la Huduma ya Maendeleo Fungani ya watu katika harakati
Shirikisho la Caritas Intarnationalis limetawanyika katika sayari zaidi ya miundo 160 ya eneo hilo ambalo limetangaza kuwa sehemu ya Tume iliyoanzishwa na Papa Francisko kwa kuongozwa na Kardinali Peter Turkson, Rais wa Baraza la Kipapa la Huduma ya Maendeleo Fungamani ya watu. Baraza hili litakuwa katika kukundi cha kwanza cha kufanya kazi ya Tume itakayojikita katika kusikiliza na kusaidia Makanisa mahalia.
Daima Caritas Internationalis inatafuta kutoa majibu
Imekuwa inajikita kuwa mstari wa mbele , anakumbushwa Bwana John na mgogoro wa dunia ambao umeletwa na virusi kwa hakika una tabia ya dharura hasa. Zaidi ya Mabaraza ya Maaskofu 140 yameeza kujibu masawali yaliyolewa kwa kuelekeza ni mahitaji yapi ya dharura kulingana na Nchi husika na ni mipango kiliyopo ya kushughulikia kuthibiti usambaaji wa janga. Bwana John ameongeza kusema “hii itaturuhusu katika mkakati kwa kushirikiana na Baraza kutoa majibu ya kutosha.
Umakini wa hali ya juu kwa nchi zenye umaskini zaidi
Akiendelea kuelezea katibu wa Caritas Internationalis amesema kuwa “umakini uko juu zaidi, kwa nchi hizo ambazo kuenea kwa janga hilo kungekuwa na athari mbaya zaidi kuliko zile ambazo tumeshuhudia huko Ulaya". Na hapa ndiyo maana kumezaliwa wazo la kuwa na “Mfuko kwa ajili ya Kujibu COVID-19", ambayo ni njia ya kukusanya michango ili kuweza kusambaza huduma kuhusu kuzuia maambukizi na kudhibiti, ufikiaji wa huduma za usafi, ugavi wa vifaa vya kinga vya kibinafsi (vibarakoa, glavu, nk), usalama wa chakula.
Maeneo mengine hawafuatilii hatua za usalama
Aidha amefafanua Bwana John kuwa “Kwa bahati mbaya kuna maeneo ambayo janga hilo linachukuliwa kuwa ni ubaya ulio mdogo kabisa hasa kwa idadi ya watu walio katika mazingira magumu. Nchini Rwanda, kwa mfano, katika maeneo mengine watu hawafuatilii hatua za usalama kwa sababu ya uhaba mkubwa wa chakula. Wanatuambia kuwa “tunapendelea kufa na Covid kuliko njaa”. Mfano mwingine unatoka Caritas Yerusalem, kule Palestina ambapo kuna hatari kubwa ya fedha za kuweza kusaidia usambazaji wa chakula na vifaa vya usafi binafsi kwa familia 500 kwenye shida .
Kuungana pamoja kwa njia ya mshikamano
Wito wa Bwana Aloysius John ni ule wa kuchangia: “ Leo sisi sote tunaunganishwa na hofu, lakini tunatakiwa hata kuuungana katika mshikamano kwa njia ya udugu ulimwenguni. Moja ya njia ya ya kushinda janga hili ni ile ya kuungana kwa pamoja ili kukabiliana na changamoto kubwa ya kibinadamu.
Hata hivyo kwa mujibu wa Caritas Internationalis inatoa taarifa kuwa inawezekana michango kutolewa kupitia tovuti yao
https://www.caritas.org/donation/covid-19-response-fund/
Vinginevyo, unaweza kutumia akaunti iliyowekwa ya Taasisi ya shughuli za Kidini IBAN: VA29001000000020179007