Misa mubashara katika Kanisa la Mtakatifu Marta inaendelea!
Kulingana na hali halisi ambayo inaendelea kujionesha kutokana na COVID-19, Baba Mtakatifu Francisko ametoa uamuzi wa kuendelea na misa kila siku asubuhi saa 1.00 kamili majira ya Ulaya hata kwa wiki ijayo katika Kanisa la Mtakatifu Marta Vatican kwa mubashara, hata Jumapili tarehe 15 Machi 2020 na kwa wiki nzima ijayo.
Kwa kuzingatia sheria zilizowekwa na marufuku ya kuwa na mikusanyiko katika harakati hizi za kuzuia kuenea kwa virusi (COVID-19), sala ya Malaika wa Bwana, tarehe 15 Machi 2020 na Katekesi ijayo ya Jumatano tarehe 18 Machi vitakuwapo mubashara. Msemaji wa Vyombo vya habari Vatican pia anabainisha kuwa katika tovuti ya Vatican News picha zitasambazwa pia Vatican itawawawezesha Vyombo vya Habari vitakavyoomba ili kufanikisha kuwafikia waamini ulimwenguni kote waweze kushiriki kwa hali yoyote.