Tafuta

Papa Francisko amefanya uteuzi mpya wa washauri wa Tume kwa ajili ya Uhusiano wa Kidini na Waislam Papa Francisko amefanya uteuzi mpya wa washauri wa Tume kwa ajili ya Uhusiano wa Kidini na Waislam  

Uteuzi wa Washauri wa Tume ya Mahusiano ya Kidini na Waislam!

Tarehe 21 Februaria 2020,Papa Francisko amewateua washauri wa Tume ya Mahusiano ya Kidini na Waislam.

VATICAN

Papa Francisko amewateua washauri wa Tume kwa ajili ya Uhusiano wa Kidini na Waislam wafautao: katoka Baraza la Kipapa la Majadiliano ya Kidini ni Padre Joseph Olawale OGUNDIPE, wa jimbo katoliki la Oyo (Nigeria); Padri  Laurent BASANESE, S.I. (Francia), Mkurugenzi wa Kituo cha Mafunzo ya Kidini ya  Chuo Kikuu cha Kipapa cha Gregoriana, Roma; Padre  Heru PRAKOSA, S.I. (Indonesia), Mshauri kwa ajili ya Majadiliano na Uislam kutoka katika Ofisi ya Katibu kwa ajili ya Uekumene na Majadiliano ya Kidini kwa Wajesuit, Profesa wa Kitengo cha Taalimungu katika Chuo Kikuu cha Sanata Dharma cha  Jogyakarta; Dk. Martino DIEZ, Mtafiti wa lugha na maandiko ya kiarabu wa Chuo Kikuu Katoliki cha Moyo Mtakatifu cha Milano na Mkurugenzi wa Kisayansi wa Mfuko wa Kimataifa wa Oasis (Italia); Dk. Timo GÜZELMANSUR, Mkurugenzi wa Christlich-Islamische Begegnungs-und Dokumentationsstelle CIBEDO wa Francofurt (Shirikisho la Ujerumani); Dk. Gabriel SAID REYNOLDS, Profesa wa Mafunzo ya Kiislam na Taalimungu katika Chuo Kikuu cha Notre Dame (Mama yetu) nchini Marekani.

 

22 February 2020, 15:59