Papa:Sinodi ya maaskofu ijayo itakuwa Oktoba 2022!
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Sonodi ya Maaskofu ijayo inatafanyika kunako mwaka 2022 ambapo taarifa zimetolewa mapema kwa ajili ya kutaka kuhakikisha utekelezaji wa Kanisa lote katika maandalizi na katika maadhimisho ya tukio hilo. Ni uamuzi wa Papa Francisko ambaye aliudhuria kikao cha mchana tarehe 6 Februari wakati wa Mkutano wa XV wa Baraza la Sekretarieti kuu ya Sinodi ya Maaskofu. Aliyetangaza tukio hili ni Katibu wa wa Baraza hilo, Kardinali Baldisseri.
Mada za siku
Katika kazi ya mkutano wa Sekretarieti ya sinodi ya Maaskofu ulioendelea hata siku ya tarehe 7 Februari 2020 wameuandaa kwa kufuata mapendekezo ya Papa Francisko kuhusu mada za kuweza kukabilinana nazo wakati wa Sinodi ijayo ya XVI ya Maaskofu pia kukabiliana na masuala ambayo yametimizwa baada ya Sinodi kuhusu vijana iliy fanyika 2018 hata yatokanayo na Wosia wa Kitume wa “Christus vivit” baada ya Sonodi hiyo.
Kusaidia wahamiaji
Papa Francikso aidha ameweza kuwakilisha hata mawazo ya uwezekano wa mada ya Sinodi ijayo ambayo bado iko kwenye mchakato wa mwisho. Vile vile katika mjadala wao wa mchana huo wamejikita katika kutazama dharura ya mshikamano kwa ndugu, kaka na dada ambao wamekumbwa katika janga la uhamiaji wa kulazimisha
Kazi ya mkutano
Mwanzoni mwa ufunguzi wa mkutano huo Katibu Mkuu Kardinali Lorenzo Baldisseri, amebainisha kwamba, kufuatia na kutangazwa kwa Kardinali Luis Antonio Tagle kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Unjilishaji wa watu, nafasi yake imewekwa Kardinali Joseph Coutts, Askofu Mkuu wa Karachi, nchini Pakistan. Katika taarifa amebainisha kuwa, Baba wa Sinodi kutoka Asia ndiye aliye nyakua kura nyingi. Kwa maana hiyo Kardinali Baldisseri baada ya kutangaza hilo aliendelea kuwakilisha matokeo juu ya mada ambazo zinaweza kukabiliwa katika kipindi chote cha mwaka 2019, ambapo kumefanyika mabaraza ya maaskofu, Sinodi za makanisa Katoliki ya Mashariki kuhusu iuris, Mabaraza ya Kipapa Katoliki na Umoja wa Mama wakuu wa mashirika. Na pia kubainisha kwamba kuhusiana na hiyo wameweza kuwa na mjadala wenye nguvu zaidi, iwe katika mkutano, pia hata katika makundi kufuatia na lugha. Aidha siku iliyofuata Kardinali Kevin Joseph Farrell, Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Walei, Familia na Maisha aliweza kuonesha shughuli zao baada ya Sinodi inayopelekwa mbele na vijana kwenye matendo dhati kuhusu Wosia wa Kitume Christus vivit baada ya Sinodi