Papa Francisko amekutana na waziri Mkuu wa Kroatia Andrej Plenković
VATICAN
Papa Francisko tarehe 6 Februari 2020 amekutana na Waziri Mkuu Bwana Andrej Plenković, wa Jamhuri ya nchi ya Croatia na baada ya mkatano huo amekutana pia na Kardinali Pietro Parolin, Katibu wa Vatican akiambatana na Askofu Mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu wa Mahusiano na Ushirikiano na chi za Nje. Katika mazungumzo na Katibu wa Vatican, wameonesha uwepo wa mahusiano mema kati ya sehemu zote mbili, na nia ya kuendeleza ushirikiano katika sekta husika.
Katika mazungumzo yao pia, wamesisitizia juu ya msingi wa jitihada za miaka 3 ya nchi ya Kroazia wa jukumu la uwenyekiti wa Baraza la Umoja wa Ulaya na kwa namna ya pekee katika kutazama changamoto ambazo zinajikita katika wakati endelevu wa Ulaya. Hatimaye wamezungumzia mantiki zinazotazama kimataifa na kikanda, ikiwa ni pamoja na hali halisi ya watu wa Kroatia walioko Bosnia -Erzegovina, uhamiaji, amani na usalama.