Papa Francisko amekutana na Rais wa Azerbaijan!
VATICAN
Tarehe 22 Februari 2020 Papa Francisko na amekutana na Rais Ilham Aliyev, wa Jamhuri ya nchi ya Azerbaijan mjini Vatican ambapo mara baada ya mkutano huo, amekutana pia na Katibu wa Vatican Kardinali Pietro Parolin akiambata na Katibu wa Mahusiano na Ushirikiano na nchi za Nje Askofu Mkuu Paul Richard Gallagher.
Kwa mujibu wa msemaji wa vyombo vya habari Vatican wanathibitisha kuwa katika mazungumzo yao na Katibu wa Vatican kwa sehemu zote mbili wamoneshwa kupendwa na maendeleo ya uhusiano wao kwa namna ya pekee suala la ushirikiano katika mantiki ya utamaduni na kupongezwa kwa shughuli zitolewazo na Kanisa Katoliki katika nchi hiyo.
Katika mantiki nyingine zilizoguswa kwa mujibu wa msemaji wa vyombo vya habari Vatican ni kuhusiana na masuala ya kikanda na kimataifa hasa juu ya umuhimu wa majadiliano ya kiutamaduni na kidini ili kukuza amani kati ya makundi tofauti ya kidini na kikabila.