Kard Parolin:uzalendo ni katika kufungamanisha wahamiaji Ulaya!
Na Sr Angela Rwezaula – Vatican
Kardinali Pietro Parolin Katibu wa Vatican katika uwakilishi wa vitabu viwili vya Civilta Cattolica” yaani ‘Ustaarabu Katoliki’ vyenye kichwa cha habari “kuwa wa kimediterania na udugu”, amesema:“Uraia ni ufunguo wa neno kwa ajili ya kukuza mchango wa ufungamanishaji kwa wale ambao wanaingia katika fukwe zetu na kuzuia matukio ya ubaguzi ambayo zaidi ni kama kutengeneza kiota cha kukuza vurugu”. Kardinali amerudi katika mada inayohusu wahamiaji wanaokuja Ulaya na Italia, ambapo akiwa pamoja na Waziri Mkuu wa Italia Bwana Giuseppe Conte wameweza kutoa hotuba zao juu ya vitabu hivyo viwili vilivyotolewa na “Civiltà Cattolica”. Bwana Conte Waziri Mkuu wa Italia amesema “suluhisho halitokani na utaifa, bali uwajibikaji wa kushirikishana kwa Ulaya nzima”.
Mwaka mmoja baada ya Hati ya Udugu kibinadamu
Kardinali Parolin amesema mkutano huo unafanyika katika kufikisha mwaka mmoja mara baada ya Kutiwa sahihi ya Abu Dhabi, kuhusu Hati ya Kihistoria ya Udugu wa Kibinadamu kwa ajili ya amani duniani na kuishi kwa pamoja kwa upande wa Papa Francisko na Sheiki Ahmad al-Tayyib, imam di Al-azhar,tarehe 4 Februari 2019.
Shughuli za wahamiaji hazitambuliki
Katika mijadala ya hivi karibuni, Kardinali Parolin amebainisha kuwa hakuonekani au kutambuliwa mchango wa wahamiaji katika maendeleo ya nchi ambazo wanakwenda, hasa Kaskazini mwa Mediterane. Na chombo hata kisheria cha kufuata ni kile cha Udugu hata kwa wale mbao wanavuka mipaka na kuingia Ulaya. Kuhusiana na masuala ya wahamiaji, Kardinali Parolin anasema “mbele yetu ulaya hatuna utambuzi na zaidi ule uhai halisi uliopo, huo hasa unatazama kwa baadhi ya nchi katika Umoja wa Ulaya na ambao wanatishia hata kufungua migawanyiko”.
Kuhusiana na mkutano wa “Kimediterania, mpaka wa amani”
Kadhalika Kardinali amekumbusha katika hotuba yake juu ya mkutano ujao utakaofanyika kuanzia tarehe 19-23 Februari 2020 huko Bari wa maaskofu wa Italia kuhusu mada ya “Mediteranea, mpaka wa amani na ambapo utahitimishwa na ziara ya Papa Francisko. Meditranea ni mahali pa makutano anasema Kardinali na wakati huo huo hata mahali pa migongano kati ya watu na utamadini wa mabara matatu kadhalika na dini kuu tatu zinazoamini Mungu mmoja. Kwa maana hiyo anakazia kwamba “lazima kutoa sauti kwa wale ambao wanatarajia na matumaini kwa watu wote. Hakuna anayebaguliwa. Ni kutafatua mahali ambapo panazaliwa thamani, utamaduni na mawazo licha ya tofauti na pia migogoro.
Kusikiliza vilio vya wakristo , waslam na wayahudi
Kardinali Parolini kadhalika ametazama mada na matatizo mengi ya mediterania, yanayotazamwa katika Hati ya udugu wa kibinadamu na kurudia kusema kuwa kile ambacho kimetendwa hadi sasa na wataalam katoliki, kiorthodox, kiislam na wayahudi ni lazima kusikilizwa sauti yao wote.