Tafuta

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limefanya Mkutano wake tarehe 21-22 Januari 2020 jijini New York,kuhusiana na suala la Nchi za Mshariki pamoja na masuala ya kipalestina Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limefanya Mkutano wake tarehe 21-22 Januari 2020 jijini New York,kuhusiana na suala la Nchi za Mshariki pamoja na masuala ya kipalestina  

Majadiliano ni muhimu katika kupata muafaka wa amani Nchi za Mashariki!

Vatican inatia moyo Jumuiya ya kimataifa ili kubaki kidete katika kuendeleza majadiliano kwa ajili ya Nchi za Masahariki.Amehimiza hayo katika hotuba yake Monsinyo Frederik Hansen,Mwakilishi wa kitume wa Kudumu Vatican katika Ofisi za Umoja wa Mataifa Jijini New York Marekani katika kikao kilichofanyika tarehe 21-22 Januari cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

Na Sr, Angela Rwezaula- Vatican

Vatican inahakikisha ushirikano wake na Jumuiya ya Kimataifa katika kuendelea kutoa msaada kwa wajili ya kuanzisha kwa mara nyingine tena kutafuta suluhu la mchakato wa majadiliano na jitihaza za amani. Hayo yamesikika katika hotuba yake Monsinyo Fredrik Hansen, Mwakilishi wa Kudumu wa Vatican katika Ofisi za umoja wa Mataifa akiwa katika  Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lililofanyika kuanzia tarehe 21-22 Januari 2020 jijini New York, kuhusiana na suala la Nchi za Mshariki pamoja na masuala ya kipalestina

Mwongozo wa maneno yake, umekuwa ni kutoka katika  hotuba ya hivi karibuni ya Papa Francisko alikukutana na wanadiplomasia  kutoka nchi za nje wanao wakilisha nchi zao Vatican, ambapo Papa Francisko alipyaisha tena juu ya wasiwasi wake wa  duniani, mahali ambapo mwanzoni mwa mwaka umefunguliwa na habari za wasiwasi wa kivita. Kwa namna ya pekee wa kuongezewa n aule wa tishio kati ya Iran na Marekani na pia ule wa Iraq na Lebanon, na si tu nchi hizo lakini katiia vita ambavyo vimegawanyika vipande vipande katika mabara yote, kuanzia kkaskazini, kwenda kusini, mashariki na magaharibi. Na kwa maana hiyo alisema tunatamani kwa dhati kuzuia hilo”.

Akiongeza umuhimu zaidi Monsinyo Hansen, amesema , hata changamoto hizo lazima zikabiliwe kwa kusilikizwa na kama ilivyo jitihada ya Jumuiya ya kimataifa kuhusu kukabiliana nazo lakini kwa njia ya zana ya majadiliano yaliyo wazi, ya kujenga yanayojikita katika misingi ambayo Umoja wa Mataifa umejisimika kwa miaka 75.

Vatican na Papa, bado bado wanaendelea kwa nguvu zote kudumisha kwa namna ya pekee umakini na Mji Mtakatifu  Yerusalemu, anaongeza Monsinyo Hansen, katika wito wake juu ya  mji wa amani. Na kwa maana hiyo anasisitizia wito  na kurudaia hivyo kama walivyo kwisha rudia mara nyingi hata kwa Shirika hili ili kuweza  kutunza, kudumisha hali ya mahali patakatifu Yerusalemu, kwa ajili ya ndugu wapendwa  Wayahudi, Wakristo na Waislam na muhimu kwa urithi wa kitamaduni wa familia nzima ya wanadamu

Dharura ambayo Jumuiya nzima ya kimataifa inapaswa ni ile jitihada ya kusaidia mchakato wa amani kati ya Isreli na Palestina ambao tayari ulikuwa imezungumzwa kwa nguvu zote na Papa Francisko katika hotuba zake na wanadiplomasia. Na pia hata katibu mkuu wa mahusiano na Nchi za nje wa Vatican katika ripoti ya Desemba mwaka jana alithbitisha hayto hayo ya dharura ambayo lazima ipatiwe suluhisho la serikali mbili kulingana na miongozo ya mwaka 1967. Kile ambacho Papa alithibitisha hivi karibuni juu ya Israeli na Palestina na kwamba  inaweza kutumika kwa mikoa yote.

 

23 January 2020, 12:00