Tarehe 17 Desemba 2019 Baba Mtakatifu anaadhimisha Siku yake ya kuzaliwa ambapo ametimiza miaka 83! Tarehe 17 Desemba 2019 Baba Mtakatifu anaadhimisha Siku yake ya kuzaliwa ambapo ametimiza miaka 83! 

Baba Mtakatifu Francisko amefikisha miaka 83:matashi mema kutoka dunia nzima!

Ni mwaka wa saba ambapo Baba Mtakatifu akisheherekea jijini Vatican siku kuu yake ya kuzaliwa tangu achaguliwe kuwa Papa.Kila kona ya dunia kwenye siku hizi zinaendelea kutuma barua na ujumbe wa matashi mema na sadaka za maombi kwa ajili ya utume wake.Kwa maana hata tarehe 13 Desemba ameadhimisha miaka 50 ya daraja la Upadre.Baba Mtakatifu Francisko hongera kwa siku yako ya kuzaliwa!

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Huu ni mwezi maalum  kwa ajili ya Baba yetu Mtakatifu Francisko, ambaye katika kipindi cha siku chache yaani ilikuwa ni tarehe 13 Desemba ameadhmisha Jubilei ya miaka 50 tangu kupewa daraja la upadre  na ambapo Jumanne tarehe 17 Desemba 2019  ametimiza miaka 83 ya maisha yake japokuwapmoa na miaka hiyo haimzuii yeye kuendelea na mbio za kuitanga Injili ya Kristo. Hata hivyo duniani kote, bado wanaendelea kumpongeza sikukuu zake... na kwa mamia elefu ya barua pepe zimefika kutoka kwa waamini wakituma matashi mema katika fura, aidha barua nyingi na michoro yao ya watoto kwa ajili ya Baba Mpendwa Mtakatifu Francisko. Kupitia mitandao ya kimamii, fabook  na instagram milioni ya watu wameza kutoa maelezo na maoni yao ya pongezi na sala kwa ajili yake".

Vile vile ujumbe wa barua kutoka kwa viongozi wa dini na serikali kwa matashi mema akianza hata kutoka kwa Baba Mtakatifu Benedikto XVI. Kati ya zawadi zilizopokelewa bila shaka ni jibu la dunia nzima kutokana na yeye anavyozidi kuendelea kuomba wasali kwa ajili ya utume wake katika kiti cha kizamani, kiti cha hekima na ambapo wakati wa Misa Takatifu na Makardinali kunako tarehe 17 Desemba 2016 alikuwa amethibitisha ni kwa jinsi gani yeye ni mwenye utulivu, mwenye furaha na nguvu.

Kwa jina la ubatizo Baba Mtakatifu Francisko anaitwa Jorge Mario Bergoglio  aliyezaliwa katika Jiji la Buenos Aires, nchini Argentina nel 1936. Ni mwana wa mhamiaji kutoka mkoa wa Piemonte nchini Italia ambaye pia kwa asili anapenda sana muziki, tangu utoto wake na  katika kazi maalum aliweza kuwa  anafuatia kwenye radio kila Jumamosi asubuhi akiwa na mama yake Regina na ndugu zake; vile vile katika damu yake anapendelea mpira wa miguuu ijapokua alieleza kuwa akiwa anachaza na marafiki zake, mara nyingi aliishia kuwa mlinda mlango daima!

Alisoma sana na kujifunza kazi mbalimbali, baadaye akapata diploma ya ufundi wa kemia, lakini upeo wa maisha yake ulikuwa ni mwingine. Aliwekwa wakfu kwa Mungu na kujikita katika huduma ya watu hivyo kunako mwaka 1958 aliingia kwenye seminari na kuchagua kuanza unovisi katika Shirika la Mpadre wa Kijesuiti. Katika kipindi hicho ndipo alikutana na nesi mmoja Sr. Cornelia Caraglio, aliy mwokoa maisha yake kwa kumshauri Dk kutumia dozi  inayofaa ili kutibu ugonjwa wa pumu.  Baba Mtakatifu Francisko katika hotuba zake mara nyingi amemtumia kama mfano mwema mtawa huyo. Katika mchakato wa kibinadamu na kumbe ulikuwapo tena  mpango wa Roho Mtakatifu ambaye alikuwa anamwona baadaye kama Kharifa wa Mtakatifu Petro

Kunako mwaka 1969 alipewa daraja la upadre. Siku hiyo Bbi yake Rosa alimkabidhi barua ikiwalekea wajuuu wake wote  ambapo aliyekuwa mdogo ni Jorge Mario, aliyoitunza brua hiyo katika kitabu chake cha sala, ikiwa na maneno yasemayo “ muwe na maisha marefu na yenye furaha. Lakini ikitokea siku moja uchungu, magonjwa au kupoteza mtu mpendwa yupo wa kuwatuliza na kuwapa nguvu na kumbukeni ile  pumzi mbele ya Taberkulo, mahali ambapo kuna mfiadini mkumbwa zaidi na mwenye haki; pia  mtazame Maria aliye chini ya msalaba  ambaye anaweza kuangusha tone la manukato juu ya majeraha ya kina na uchungu”

Kunako mwaka 1973 alitangazwa kuwa mkuu wa Provinsu ya wajesuiti huko Argentina. Kunako mwaka 1992 alichaguliwa kuwa askofu. Na 28 Februari 1998 akatangwa kuwa Askofu Mkuu wa Buenos Aires na kiongozi  mkuu wa Kanisa la Argentina. Katika uchaguzi wa tarehe 21 Februari  2001  Mtakatifu Yohane Paulo II alimchagua kuwa Kardinali. Katika fursa hiyo Mtakatifu Paulo II alitamka manenoa haya: " Leo hii asubuhi hii Roma  Katoliki inawazunguka makardinali wapya na kuwakumbatia kwa upendo mkuu, kwa utambuzi kuwa wanaandika ukurasa mpya wenye maana katika historia ya maisha yao.

Katika tukio jingine tena muhimu linalokumbwa zaidi ni lile la tarehe 13 Machi 2013 ambapo Kardinali  Jorge Mario Bergoglio Askofu Mkuu wa Buenos Aires alichaguliwa kuwa Papa,  Mwamerika wa kwanza na Mjesuit wa kwanza, na wakati huo huo Papa wa kwanza kuchagua jina la Francisko kama Mtakatifu wa Assisi ambaye alikuwa na marafiki zake maskini, watu walio wa mwisho, wagonjwa,  viumbe vyote vya ardhi, dada Mwezi na kaka Jua na katika moyo wa amani kati ya watu na mataifa.  Na ndiyo marafiki hao hao waliompendeza  katika maneno ya na ishara za Huduma yake kama Papa! Hongera sana Baba Mtakatifu Francisko katika siku yako ya kuzaliwa!

17 December 2019, 10:37