Mhs.Padre Joseph Kizito ni Askofu mpya wa Jimbo la Aliwal-Afrika Kusini!
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Baba Mtakatifu Francisko amemteua Askofu wa Jimbo Katoliki la Aliwal, Afrika ya Kusini Mheshimiwa Padre Joseph Kizito wa jimbo hilo hilo, ambaye hadi uteuzi wake alikuwa ni Makamu Askofu na Paroko wa Aliwal. Mheshimiwa Padre Joseph Kizito alizaliwa tareh 2 Julai 1967 Kampala Uganda. Alisomea mafunzo ya Falsafa katika Seminarti Kuu ya Mtakatiufu Augustine (Lesotho), Taalimungu katika Seminari ya Mtakatifu John Vianney, Pretoria, Afrika Kusini. Alipewa daraja la upadre kunako tarehe 27 Septemba 1997 na kuwekwa katika Jimbo Katoliki Aliwal, Afrika Kusini.
Shughuli za utume wake Padre Mteule
Katika shughuli zake za kitume ni kuanzia 1997-1998 amekuwa Paroko msaidizi wa Parokia ya Mtakatifu Francis Xavier; 1998-2003 kuwa Parokia ya Mtakatifu Augustine huko Dordrecht; 2003-2013 kuwa katika Paroko wa Parokia ya Sterkspruit; Tangu 2008 amekuwa Makamu wa Askofu katika Jimbo Katoliki Aliwal; na tangu 2013 ni Paroko wa Kanisa Kuu la Aliwal.