Ratzinger kwa makardinali wapya amewasihi wakumbuke thamani ya uaminifu kwa Papa!
Tarehe 5 Oktoba 2019 majira ya jioni hivi, mara baada ya kuhitimishwa madhimisho ya kusimikwa kwa makardinali wapya, Baba Mtakatifu Francisko pamoja na Makardinali wapya wamekwenda kwa Bus ndogo hadi kwenye Monasteri ya “Mater Ecclesiae” mjini Vatican ili kukutana na Baba Mtakatifu Mstaafu Benedikto XVI. Hayo ni kwa mujibu wa msemaji Mkuu wa Vyombo vya habari Vatican Dk. Matteo Bruni.
Baada ya salam fupi pia kuwakumbusha makardinali wapya juu ya thamani ya uaminifu kwa Papa, Baba Mtakatifu Mstafu Benedikto XVI pamoja na Baba Mtakatifu Francisko wamewabariki makardinali kwa kwa baraka yao. Na hatimaye Makardinali wapya wamerudi katika ukumbi wa Papa Paulo VI na katika Nyumba ya Kitume kwa ziara ya faragha na wakati huo huo Baba Mtakatifu Francisko akarudi nyumbani kwake katika Nyumba ya Mtakatifu Marta.