Askofu Grech ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu mwambata wa Sinodi ya Maaskofu!
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Askofu Mario Grech, wa jimbo la kisiwa cha Malta ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu Mwambata wa Sinodi ya Maaskofu ambaye atashirikiana na Kardinali Lorenzo Baldisseri, ambaye ni Katibu Mkuu wa Sinodi ya Maaskofu. Hata hivyo ni Kardinali Baldisseri mwenyewe, aliyetangaza saa sita kamili tarehe 2 Oktoba 2019, siku chache kabla ya kuanza Sinodi kwa ajili ya Kanda ya Amazonia inayotatajiwa kufunguliwa tarehe 6 Okotba 2019. Akizungumza na waandishi wa habari amesema Askofu Mario Grech, wa jimbo la Gozo pia ametangazwa kuwa Msimamizi wa Kitume katika jimbo hilo hilo hadi atakapoteuliwa Askofu mwingine. Katibu Mkuu mwambata atabeba majukumu moja kwa moja akiwa karibu na Kardinali Baldisseri ili kumfanya awe na uzoefu, utambuzi mzuri na washiriki wake na kupata ufahamu wa michakato mbalimbali ya uendeshaji wa mikutano na hali halisi ya ustadi wa kazi ukatibu mkuu katika Sinodi.
Kardinali Baldisseri amesema, Askofu Grech atakamilisha ofisi yake ya kuwa Katibu Mkuu wa Sinodi hadi hapo Yeye atakapo ng'atuka katika utumea wakati atakapo timiza miaka 80 kunako mwezi Septemba 2020. Aidha Kardinali Baldisseri amehitimisha kwamba, kutangazwa kwake kama Katibu mwambata wa Sekretarieti ya Sinodi ya Maaskofu pia atashiriki kama mjumbe katika Sinodi ijayo itakayoanza tarehe 6 Oktoba 2019. Askofu Grech alizaliwa tarehe 20 Februari 1957 huko Qala. Askofu Grech alipewa daraja la Upadre kunako mwaka 1984 na kutangazwa kuwa Askofu wa jimbo la Gozo huko Malta, kunako Novemba 2015 na Baba Mtakatifu benedikto XVI.