Papa akutana na Patriaki Bartholomeo I mjini Vatican!
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Baba Mtakatifu Francisko amekutana mjini Vatican na Patriaki Barthomoleo I ambapio katika mkutano wao pia wamebadilishana zawadi, baadaye ikafuatia chakula cha mchana kwa pamoja na wawakilishi wake katika nyumba ya Mtakatifu Marta mjini Vatican, tarehe 17 Septemba 2019. Kabla ya mkutano huo, kwa mwaliko wa Askofu Semeraro, anbaye ni Katibu wa Baraza la Makardinali, Patriaki amewasalimia kwanza wajumbe wa Baraza la Makardinali ambao wameanza Mkutano wao kuanzia tarehe 17 hadi 19 Septemba. Katika mazungumzo nao amesisitizia juu ya thamani ya mikutano ya Kanisa la Kiorthodox, na zaidi kuwahakikishia uwepo karibu nao katika sala zake.
Hata hivyo kwa mujibu wa msemaji mkuu wa Vatican ni kwamba kabla ya mkutano wa siku hiyo, Baba Mtakatifu Francisko alikuwa amemtumia barua Patriaki. Katika barua hiyo, Baba Mtakatifu ameweka bayana maana ya zawadi ya hivi karibuni ya baadhi ya masalia matakatifu ya Mtakatifu Petro kwa Kanisa la Constantinopoli, na ambayo kwa sasa yamewekwa karibu na masalia ya Mtakatifu Andrea. Hii ni kutaka kuthibitisha kwamba chombo kinacho tunza masalia aliyuo mzawadia Patriaki wa Costantinopoli, ndani mwake kuna aina tisa za mifupa ya Mtakatifu Petro, na ambayo ni sehemu ya mifupa iliyo kuwa imetunzwa katika kifaa maalum jijini Vatican.