Askofu mkuu Ayuso Guixot anaelezea juu ya matunda ya kwanza ya Hati ya Udugu wa kibinadamu kwamba ni pamoja na kuundwa Kamati kuu ya utekelezwaji wa hati hiyo Askofu mkuu Ayuso Guixot anaelezea juu ya matunda ya kwanza ya Hati ya Udugu wa kibinadamu kwamba ni pamoja na kuundwa Kamati kuu ya utekelezwaji wa hati hiyo  

Askofu Ayuso Guixot: Matunda ya Hati ya Udugu wa Kibinadamu yaanza kuonekana! Kiu ya amani!

Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya majadiliano kidini, Askofu Miguel Ángel Ayuso Guixot, amejaribu kuelezea juu ya tathimini ya matunda ya kwanza ya Hati ya Udugu wa Kibinadamu iliyotiwa sahini mwezi Februari mwaka 2019 huko Abu Dhabi na Baba Mtakatifu Francisko pamoja na Imam mkuu wa Al Azhar. Matunda hayo ni pamoja na kuundwa kwa Kamati kuu ya utekelezwaji wa hati hiyo.

Na Sr. Angela Rwezaula - Vatican

Wakati wa mahojiano na Vatican News Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya majadiliano kidini Askofu Mkuu Miguel Ángel Ayuso Guixot,amejaribu kuelezea juu ya tathmini ya matunda ya kwanza ya Azimio la pamoja kuhusu Udugu wa kibinadamu uliotiwa sahini mwezi februari mwaka huu huko  Abu Dhabi na Baba Mtakatifu Francisko akiwa na  Imam mkuu wa di Al Azhar. Askofu Mkuu Guixot amesema  mazungumzo ya ukidini ndiyo njia bora ya kuweza kukabiliana na uovu wa itikadi kali. Hata hivyo amesisitiza juu ya kuanzishwa hivi karibuni Kamati kuu mpya kwa ajili ya utekelezwaji wa Hati ya Udugu wa kibinadamu na ambayo ni hatua ya kwanza ya mchakato mzima wa utekelezaji. Kwa upande wake amesema Kamati hiyo na ambapo ametiwa moyo na Baba Mtakatifu Francisko ni mfano wa dhati katika jitihada za viongozi wa kidini ili waweze kujenga  madaraja, ujenzi wa mazungumzo na kishinda vishawishi vya kujifungia binafsi ambavyo pia vinafafanua katika malumbano dhidi ya maendeleo.

Kuundwa kwa Kamati kuu ni tendo lenye maana

Kuundwa kwa Kamati kuu ni tendo la maana sana amebainisha, na hii ni kama inavyosomeka katika maelezo yaliyo andikwa wakati wa kuzaliwa  hati hiyo na kwamba ni kuhamasisha mawazo yaliyomo kwenye hati ya Udugu kibinadamu kwa sababu ni tamko la pamoja katika jitihada za kuunganisha binadamu na kufanya kazi kwa pamoja kwa ajili ya amani duniani na mwisho ili kuweza kuhakikisha kuwa, vizazi vijavyo vinaweza kuishi katika hali ya kuheshimiana na kuishi vema pamoja. Lengo hili ni bora!  Aidha anamshukuru mrithi wa Abu Dhabi, Sheikh Mohamed bin Zayed Al Nahyan ambaye amefanya kazi ili kuwa na maendeleo ya  mpango  na  kutekeleza malengo ya hati ya  Udugu wa Kibinadamu ya Abu Dhabi. Aidha anamshukuru Baba Mtakatifu Francisko na Imam Mkuu wa Al- Azhar kwa sababu ya maneno na ushuhuda wao ambao umewezesha kile alichosema mrithi katika dibaji ya Kamati kuu.

Nini kilimvutia katika ziara ya Baba Mtakatifu katika nchi za uarabuni

Kuhusiana na suala la kile kinacho mvutia zaidi katika utashi wa mazungumzo ya Baba Mtakatifu kwenye  ziara katika nchi za  Uarabuni awali ya yote anatoa shukrani kwa ajili ya jitihada za uhamasishaji wa mazungumzo!  Na kwa hakika amabainisha kwamba ni kwa mapapa wote  waliomtangulia Baba Mtakatifu Francisko kuhusiana na mazungumzo yao ya heshima na urafiki, kwa maneno na matendo. Zaidi ameongeza kusema hawakosi kamwe kutoa ushauri katika dunia nzima na kwa watu wote wenye mapenzi mema  na hasa katika kuhamasisha mambo matatu:udugu, amani na kuishi vizuri. Ameongeza kusema kuwa watu wote hawapaswa kusahau kuwa mambo haya matati ndiyo nguzo msingi iwapo tunataka kweli kupona majeraha  ya dunia yetu. na ndiyo kitabu cha mwanzi kama ABC na cha wakati endelevu. Ni wengi walioshirikiana katika mpango wa kuandaa hati hiyo amesema, na kwa hakika wanakukwa katika sehemu ya mwisho ya Hati hiyo.

Kamati kama tamko inazaliwa na kutokana na mazungumzo kati ya waislam na wakristo, kuna uwezekano wa kufikiria upanuzi wa dini nyingine

Askofu Mkuu Guixot akielezea muktadha kuhusu kamati iliyozaliwa kutokana na  tamko amesema, Tamko linazaliwa na mazungumzo kati ya waislam na wakristo kwa  mantiki ya mkutano mkuu juu ya Udugu wa  Kibinadamu. Na ndiyo mantiki ya ulimwengu ambayo ndiyo ujumbe wa tamko lililo enea dunia kote na ambalo ni  dirisha jipya linalojifungua kwa mantiki ya Roho ya Assisi. Kwa matokeo zaidi ya nani, wapi na lini, katika ujumbe wa ulimwengu kuhusu udugu wa amani na kuishi pamoja ni jumuishi na kushirikishwa kwa wote waamini wa dini zote, pamoja na watu wote wenye mapenzi mema. Kwa mfano amesema, mwezi ujao Septemba, ataudhuria mkutano wa kimataifa  huko Madrid, Spain mkutano kuhusu watu na dini, ulioandaliwa na Jimbo Kuu Katoliki la Madiri na Jumuia ya Mtakatifu Egidio. Katika meza ya mduara ya Mkutano huo watazungumzia kwa dhati  juu ya tema hii ya udugu wa kibinadamu pamoja na wahusika wa dini mbalimbali.

Dini zinazokiri Mungu mmoja lazima kufanya kazi pamoja na nyingine zote

Jambo pia muhimu ambalo amekazia amesema dini zinazomkiri Mungu mmoja  pamoja na zingine zote zitatakiwa kufanya kazi pamoja kwa sababu ndicho kilichosainiwa na Baba Mtakatifu Francisko na   Imam Mkuu, kwamba kila sehemu iweze kuenea ile hali ya kuishi kwa amani na wema wa kibinadamu. Kutokana na hili Kamati mpya itakuwa chombo muhimu sana amesema. Na kwa  sababu hii  ametumia fursa hiyo kusasisha shukrani zake binafsi  kwa tathmini yenye thamani ambayo Imamu Mkuu, ndugu yao wa Al Azhar amefanya katika vyombo vya habari na ambayo anaungana nao kwa niaba ya Baraza la Kipapa la Majadiliano ya Kidini na Yeye akiwa kama rais wake.

27 August 2019, 14:16