Katika uwasilishaji wa Ripoti ya Matokeo ya Hospitali ya Kipapa ya Bambino Gesù,Kardinali Pietro Parolin anawapongeza wote ambao wametoa mchango wao kutimiza  ufanisi wa Hospitali hiyo Katika uwasilishaji wa Ripoti ya Matokeo ya Hospitali ya Kipapa ya Bambino Gesù,Kardinali Pietro Parolin anawapongeza wote ambao wametoa mchango wao kutimiza ufanisi wa Hospitali hiyo 

Kard.Parolin anakumbusha wajibu wa kulinda daima maisha katika juhudi za Hospitali ya Bambino Gesù!

Hospitali ya Kipapa ya Watoto Bambino Gesù imewakilisha Ripoti tarehe 24 Julai 2019 kwa kuonesha matokeo ya shughuli za Afya na sayansi katika takwimu kijamii kwa mwaka 2018 mbele ya Kardinali Pietro Parolin Karibu wa Vatican.Katika ripoi hiyo inaonesha kuongezeka kulazwa kwa wagonjwa,kuongeza huduma za vituo vya nje,upandikizaji wa viungo na uzalishaji wa kisayansi katika ngazi za juu.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Inawezakana kutenda wema na kuutenda vema. Hii inajionesha katika idadi kubwa ya shughuli za afya na kisayansi kwenye takwimu za ripoti ya mwaka 2018 ya Hospitali ya kipapa ya Watoto  “Bambino  Gesu”, iliyowakilishwa tarehe 24 Julai 2019 katika makao ya Mtakatifu Paulo jijini Roma. Mkutano huo umefunguliwa na Rais wa Hospitali hiyo Bi Mariella Enoc ambaye baada ya utambulisho imefuatia hotuba ya Kardinali Pietro Parolin Katibu wa Vatican.

Hotuba ya Kardinali Pietro Parolin

Katika hotuba yake Kardinali Pietro Parolin anasema, matokeo yaliyopatikana yako mbele ya macho ya wote na kuwapongeza wale wote ambao wametoa mchango wao kutimiza ufanisi huo. Katika fursa ya maadhimisho ya miaka 150 tangu kuanzishwa kwa Hospitali ya Bambino Gesù, Baba Mtakatifu Francisko katika barua yake alionesha kuwa “anayekita kutoa matibabu kwa walio wadogo zaidi yuko katika sehemu ya Mungu na anashinda utamaduni wa kibaguzi”. Katibu wa Vatican amekumbuka maneno ya Baba Mtakatifu huku akitafakari matokeo ya ufanisi wa jengo la Afya la Vatican.  Ni ripoti bora zaidi inayohusu shughuli za afya, shughuli za kisayansi na ripoti ya kijamii ikiwa na mipango yake ya kibinadamu katika nchi 10. Kardinali Parolin amewaalika wasisimame kamwe! “Ni muhimu kwamba lengo hili bora lisijikunjike na  tusisahau kamwe kuwa thamani ya mafanikio yaliyopatikana hupimwa katika uwezo wa kuboresha ubora wa utunzaji na usaidizi. Watoto, vijana na familia zao wako na lazima wabaki katika mioyo ya kila shughuli, kila mchakato na kila hatua inayofanywa”.

Wazo kwa ajili ya Vincent Lambert: kulinda maisha daima

Hata hivyo katika hotuba yake, Kardinali Parolin amewaalika “kushinda hatari ya migawanyiko na ukimbele mbele na kuwashauri kila mmoja ajikite katika nafasi yake  kwa utambuzi na unyenyekevu”. Na akigusia juu jambo la Vincent Lambert amekumbusha kuwa ndani ya usimamizi imara na busara, inawezekana kukuza uendeshaji. Aidha , “Ninafikiri kazi iliyoanzishwa kwa ajili ya Taasisi ya Saratani na Upandikizaji wa viungo au kubuni chumba cha kukaa watoto wachanga; ni kwa jinsi gani katika siku hizi kuwa muhimu sana na zaidi baada ya kifo cha Vincent Lambert, ambaye ameamsha  tena ndani mwetu kumbukumbu ya watoto Alfie Evans na Charlie Gard. Kwa maana hiyo ameongeza kusema”,kutokana na hiyo ameongeza kusema: “ tunalo jukumu la kuthibitisha kuwa kuna magonjwa ambayo hayaponi, lakini hakuna magonjwa yasiyoweza kutibika. Na ili kuweza kutibu  haina maana tu ya kuponyesha lakini hata ile ya kusindikiza na kulinda. Na kama alivyothibitisha Baba Mtakatifu Francisko  wakati akionesha uchungu wake wa tukio hilo alisema: “ Ni mungu peke yake mkuu wa maisha kuanzia mwanzo hadi kifo cha kawaida, ni wajibu wetu kuyalinda maisha daima”.

Kuhusiana na wasiwasi  wa kibinadamu nchini Siria

Katibu Mkuu wa Vatican Kardinali Pietro Parolin akijibu swali kando ya  mkutano huo kwa mwandishi wa habari kuhusiana na mada ya Siria na barua ya Baba Mtakatifu iliyomfikia Rais wa Siria Assad, amerudia kusema yale ambayo tayari alikuwa amethibitisha katika mahojiano na Vatican news, kuhusu wasiwasi wa Vatican ambao ni mkubwa kwa ajili ya maisha ya kibinadam nchini humo.

Shughuli za kliniki na kisayansi

Naye Mkurugenzi wa Kituo cha Afya Massimiliano Rapon na Mkurugenzi wa Kisayansi Bruno Dallapiccola na Murugenzi Mkuu Ruggero Parrotto wakati wa uwakilishaji wa shughuli zao, wamewekwa mwanga zaidi kuhusu  matokeo mema ya Hospitali ya Vatican. Bambino Gesù kwa hakika imepiga hatua kubwa hasa kuwa karibu na milioni mbili ya vituo nje vya kutoa huduma na wakati huo huo wagonjwa wa kulala ni 29,000. Kwa kuongezea zaidi kile kitengo cha kupandikiza viungo. Kwa hakika hii ni  hospitali pekee katika bara la Ulaya  yenye uwezo wa kujibu hitaji la aina yoyote ya kupandikiza viungo na  ambayo imejitofautisha na shughuli za operesheni  324 za seli na tishu.

Hata hivyo pia imejihusisha kuonesha matokeo katika matibabu ya magonjwa nadra  au adimu, kwa kesi za magonjwa mapya 21 adimu yaliyotambuliwa na zaidi ya wagonjwa 13,000 wenye  magonjwa yasiyo ya  kawaida waliyo fuatilia. Katika jitihada hizi inaongezeka hata kazi kubwa ya  utafiti na ambayo imewezesha kutoa uchapishaji wa makala 679, kwa kukadiriwa na vidokezo vya 2968 vya  Impact Factor Raw (IFG), yaani njia ya kupima thamani ya masomo ya kisayansi yaliyozalishwa. Kwa maana hiyo ni Shukrani kwa Taasisi yenye kushika nafasi ya tatu katika mtandao wa Taasisi za Hopitali za kulala na utunzaji zenye kuwa na tabia ya Hospitali ya kisayansi (IRCCS) na ni ya kwanza kati ya hospitali za watoto nchini Italia.

Ni Hospitali ya makaribisho

Hospitali ya watoto Bambino Gesù inakaribisha karibia familia zenye wagonjwa wa kulala 4,500  na 2,100 wa familia zinazofuatiliwa na huduma ya kijamii. Ni wagonjwa 62 wa  msaada wa kibinadamu walio karibishwa kutoka nchi 68. Hii ni ishara ya kuwa hospitali hiyo ni  wazi, inayokaribisha na kuwa na mshikamano. Na katika kusheherekea mafanikio hayo na miaka 150 tangu kuanzishwa kwa hospitali hiyo, tarehe 20 Novemba ijayo, wanatarajia kuandaa tukio liitwalo:  usiku wa nyota za mtoto Yesu (le stelle del Bambino Gesu’) katika Ukumbi wa Paulo VI , kwa lengo la kukusanya fedha za ujenzi wa Taasisi mpya ya Saratani na upandikizaji wa viungo.

25 July 2019, 10:22