Hebdomada Papae: Radio Vatican inakuletea Matangazo kwa lugha ya kilatino
Na Sr Angela Rwezaula – Vatican
Tarehe 8 Juni 2019, masafa mapya ya Radio Vatican itatangazwa kipindo kiitwacho Hebdomada Papae, notitiae vaticanae latine redditae’, yaani habari za wiki za shughuli za Baba Mtakatifu na Vatican kwa lugha ya kilatino. Hiki ni kipindi kipya kabisa cha habari za wiki kwa lugha ya kilatino kwa dakika 5, ambazo zitawekwa pia katika podcast ya Vatican News. Hii imeundwa kwa ushirikiano wa uhairiri wa Radio Vatican na Ofisi ya Katibu wa Vatican kwenye kitengo cha tafsiri za barua za Kilatino na Tweet za Acount ya @Pontifex_ln.
Matangazo ya kila Jumamosi kwa dak 5 saa 6.32 na marudio Jumapili jioni
Habari mpya za matangazo ya radio kwa lugha ya kilatino ambayo yatadumu kwa dakika tano, yatahaririwa na Alessandro De Carolis, ambayo yatatangazwa kila Jumamosi kwenye masafa ya Radio Vatican (kwa upande wa wa Italia ni saa 6.32 na kurudiwa tena kila Jumapili saa 11.30 jioni masaa ya Ulaya).
Tornielli: ni habari halisi za radio halisi; changamoto kwa siku zijazo
Naye amkurugenzi wa uhariri wa Radio Vatican, Bwana Andrea Tornielli akifafanua juu ya kuanzishwa kwa matangazo haya amesema: “kwa kuanzishwa kipindi hiki cha kila wiki, tunataka pia kufufua hata habari katika lugha rasmi ya Kanisa Katoliki ambayo tayari ipo kila siku katika mzunguko wa Radio Vatican hasa wakati maadhimisho ya misa takatifu ya kila asubuhi kwa lugha ya kilatino”. Vilevile amethibitisha: "hii ni huduma ya habari na halisi. Hatukufikiria kama ni kufanya kumbukumbu ya wakati uliopita, bali ni kama changamoto kwa siku zijazo”.