Hija ya Kitume:Papa amefika Macedonia Kaskazini katika ishara ya Mama Teresa!
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Tarehe 7 Mei 2019 Baba Mtakatifu Fracinsko amefika mji wa Skopje nchini Macedonia ya Kaskazin, ikiwa ni hatua yake ya pili ya mwisho wa ziara yake ya 29 ya kitume baada ya Bulgaria. Baba Mtakatifu ameanza safari asubuhi saa 2.33 ,saa mahalia ikiwa ni saa 7.33 nchini Italia, baada ya kumaliza sherehe za kuagana na Waziri Mkuu wa Bulgaria Bwana Borisov.
Baada ya safari karibu ya nusu saa kwa ndege, Baba Mtakatifu ametua uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Skopje mahali ambapo amekuta rais wa Jamhuri, Gjorge Ivanov,akimsumbiri na watoto wakiwa wamevaa nguo za utamaduni wamempatia mkate, chumvi na maji ambapo Baba Mtakatifu ameshirikishana na wote waliokuwa karibu naye. Wakati akifika katika uwanja wa kimataifa wa Skopje uwakilishi wa waamini katoliki walikuwapo ambao wamemsalimia Baba Mtakatifu Francisko kwa makofi kwa vigelela hadi anamfikia waziri Mkuu.
Hii ni hatua ya kwanza ya siku nchini Macedonia ya Kaskazini ambapo Baba Mtakatifu amepokelewa na sherehe rasmi za kumkaribisha saa 3.15 katika uwanja wa Ikulu na kutembelea kwa faragaha Rais wa nchi Bwana, Gjorge Ivanov,saa 3.30, mkutano na waziri Mkuu Zoran Zaev. Na saa 3.45 viongozi wa nchi wa kidiplomasia katika ukumbi mkuu wa rais. Saa 4.20 Baba Mtakatifu atatembelea Kumbu kumbu ya mama Teresa wa Kalcuta wakiwepo viongozi wa dini na mkutano na maskini 100 wanaohudumiwa na Watawa wamisionari wa Upendo wa shirika la mama Taresa wa Kalcuta.
Baba Mtakatifu ataadhimisha misa Takatifu saa 5.30 katika Uwanja wa Macedonia na baada ya chakula cha mchana saa 7.30 na alioambata nao, itafuatia mkutano wa kiekumene na kidini saa 10.00 jioni na vijana wa Kituo cha kichungaji, ambapo Baba Mtakatifu atahutubia kabla ya sala ya Mama Taresa isemayo: “Unahitaji mikono yangu ee Bwana”. Saa 11.00 atakutana na mapadre na familia zao na watawa katika Kanisa Kuu. Baaada ya sherehe za kuagwa katika uwanja wa kimataifa wa Skopje, Baba Mtakatifu anatarajia kuanza safari ya kurudi Roma saa 12.30 na matarajio ya kufika saa 2.30 usiku mjini Roma.