Mwezi Septemba Papa anafanya ziara nchini Msumbiji,Madagascar na Mauritius
Na Sr. Angela Rwezaula - Vatican
Kwa mujibu wa Msemaji Mkuu wa mpito wa vyombo vya habari Vatican,Dkt Alessandro Gisotti, tarehe tarehe 27 Machi 2019 ametoa taarifa ya kwamba Baba Mtakatifu Francisko atafanya ziara yake ya kitume nchini Msumbiji, Madagascar na Mauritius kuanzia tarehe 4-10 Sepemba 2019. Dkt. Gisotti anathibitisha kwamba:"kwa kupokea mwaliko kutoka kwa wakuu wa nchi na maaskofu wa nchi hizo zote, Baba Mtakatifu Francisko atatimiza Ziara yake ya Kitume nchini Msumbiji, Madagascar na Mauritius kwa kutembelea miji ya Maputo Msumbiji, Antananarivo nchini Madagascar na Port Louis huko Mauritius". Hata hivyo ratiba nzima ya ziara yake itatolewa muda mwafaka.
Matumaini, amani na mapatano ndiyo kauli mbiu ya ziara ya kitume nchini Msumbiji
Matumaini, amani na mapatano ndiyo kauli mbiu inayoongoza ziara ya kitume ya Papa nchini Msumbiji. Katika ramani ya nchi inaonesha, Baba Mtakatifu na njiwa ikiwa ni ishara ya amani. Mikono miwili inamaanisha makaribisho ya nchi ya Msumbiji kwa Baba Mtakatifu na hata ujumbe wa matumaini, amani na mapatano unaobebwa na watu wa msumbiji. Wakati huo huo rangi katika nembo zipo tano za bendera ya Msumbiji. Kijani inamanisha matumaini, nyekundu ina maana ya mapatano na rangi nyeupe ina maana ya amani, wakati rangi ya njano ikimaanisha rangi ya Vatican.
Kisiwani Madagascar ni mpanda amani na matumaini
Mpandaji wa amani na matumaini ndiyo kauli mbiu itakayo ongoza ziara ya Baba Mtakatifu Francisko katika Kisiwa cha Madagascar. Katika nembo ya nchi inawakilisha mnazi wa msafiri, mafuta na mbuyu. Hata hapa inaonesha Baba Mtakatifu na baadhi ya watakatifu, mashahidi wa nchi, wamisionari na mashuhuda wa imani hadi kifo dini.
Katika nembo ya Mauritius ya ziara ya Papa anaongozwa na kauli ya mhujaji wa amani
Na kwa kuhitimisha na kauli mbiu za ziara nchini Mauritius, “Papa Francisko ni mhujaji wa amani”, ndiyo maneno yaliyo chaguliwa kutengeneza kaulimbiu ya ziara yake huko Mauritius. Katika Bendera ya Mauritius,inaonesha Papa akiwasalimia watu!