Ask.Mkuu Novatus Rugambwa Balozi mpya wa New Zealand!
Na Sr. Angela Rwezaula - Vatican
Baba Mtakatifu Francisko amemteua Balozi wa Vatican nchini New Zealand na mwakilishi wa Kitume wa Bahari ya Pwani, Mheshimiwa sana Askofu Mkuu Rugambwa. Kabla ya uteuzi wake alikuwa ni Balozi wa Vatican huko Honduras.
Askofu mkuu Novatus Rugambwa alizaliwa tarehe 8 Oktoba 1957, Katika Jimbo Katoliki Bukoba, Tanzania. Baada ya masomo na majiundo yake ya kikasisi, alipewa daraja Takatifu ya Upadre kunako tarehe 6 Julai 1986. Baada ya kufanya kazi mbali mbali katika Balozi za Vatican, kunako tarehe 6 Februari, 2010, Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI, alimteua kuwa Askofu mkuu na Balozi wa Vatican nchini Angola, Sao Tome na Principe. Na tarehe 5 Machi 2015 aliteuliwa kuwa balozi wa Vatican huko Honduras, ambapo sasa tarehe 29 Machi 2019, ameteuliwa kuwa Balozi wa Vatican huko New Zealand na mwakilishi wa Kitume wa Bahari ya Ocean.