Benedetta Bianchi Porro ni mmoja kati ya walikubaliwa kutangazwa wenye heri wapya wa Kanisa Benedetta Bianchi Porro ni mmoja kati ya walikubaliwa kutangazwa wenye heri wapya wa Kanisa 

Papa aridhia kutangazwa kwa wenyeheri wapya wa Kanisa

Baba Mtakatifu Francisko ameridhia kutangazwa kwa wenye heri wapya wa Kanisa na kati yao wapo walei wawili wa Italia, Edvige Carboni na kijana Benedetta Bianchi Porro pamoja na mashidi 11 waliouwawa kwasababu ya kutetea imani yao katika vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Uhispania

Sr. Angela Rwezaula - Vatican

Tarehe 8 Novemba 2018, Baba Mtakatifu Francisko, amekutana na na Kardinali Angelo Becciu Rais wa Braza la Kipapa la Kuwatangaza watakatifu, na kuridhia kuwatangaza baadhi kuwa wenye heri  na kuwatambua wengine fadhila za kishujaa kuwa watumishi wa Mungu kumi.

Utambuzi wa wafiadini 11 watakaotangazwa kuwa wenyeheri

Wafia dini watatangwaza wenye heri 11 ambao ni Angelo Cuartas Cristóbal na  na wenzake  8, waseminali wa Oviedo, waliouwawa kwa ajili ya kutetea imani yao huko  Oviedo  nchini Uhispania kati ya 1934 na 1937; Mariano Mullerat i Soldevila, Meli na baba wa familia alizaliwa Mtakatifu Coloma de Queralt (Uhispania) tarehe 24 Machi 1897  na kuwawaHuko  El Pla, karibu na  Arbeca (Uhispania) tarehe 13 Agosti 1936; Giacomo Alfredo Miller, Ndugu  wa Shirika la Shule ya Wakristo aliyezaliwa  Stevens Point (Marekani  tarehe   21 Septemba 1944  aliuwawa kwa sababu ya kutetea imani yake huko Huehuetenango (Guatemala) tarehe  13 Februari 1982.

Baba Mtakatifu amerithia pia  fadhila za kishujaa kwa watumishi wa Mungu 10

Hawa ni Giovanni Jacomo, Askofu Mkuu wa  Mocisso,aliyekuwa pia askofu wa Caltanissetta; alizaliwa Ragusa (Italia) tarehe 14 Machi  1873 na kifo chake tarehe 25 Machi 1957; Alfredo Maria Obviar,  Askofu wa Kwanza wa  Lucena  na Mwanzilishi wa Shrikia la Wamisionari wa Makatekisti wa Mtakatifu Teresa wa Mtoto Yesu. Alizaliwa huko Lipa (Ufilippini) itarehe 29 Agosti 1889 na kifo chake huko Lucena (iilippini) il 1° ottobre 1978; - Giovanni Ciresola, Padre wa Jimbo, Mwanziloshi wa Shirika la Maskini wa Dada wa Damu Azizi . Karamu ya Upendo; alizaliwa huko Quaderni ya  Villafranca (Italia) tarehe  30 Mei 1902  na kifo chake huko  Quinto ya Valpantena (Italia) tarehe  13 Aprili 1987;  Luigi Bosio, SPadre wa Jimbo; alizaliwa huko Avesa (Italia) tarehe  10 Aprile 1909  na kifo chake huko Verona (Italia) tarehe  27 Januari 1994.

Luigi Maria Raineri, mwanashirika wa Shirika la Mtakatifu Paulo (Wabarnabiti); alizaliwa huko Torino Italiwa tarehe 19 Novemba 1895 na kifo chake huko Crespano( Italia) tarehe 24 Novemba 1918; -Raffaella wa Mateso jina ubatizo  Raffaella Veintemilla Villacís), Mwanzilishi wa Shirika lwa Wagostiniani Wana wa Mwokozi Mtakatifu; alizaliwa tarehe 22 Machi  1836  na kifo chake huko Lima (Peru) tarehe 25 novemba 1918; Maria Antonia wa  Gesù (jina la ubatizo: Maria Antonia Pereira y Andrade), Mtawa wa Shirika la wakarmeli. Alizaliwa  huko El Penedo (Uhipania) tarehe 5 Oktoba 1700 na kifo chake huko Santiago ya  Compostela (Uhipania) tarehe 10 Machi 1760.

Arcangela Badosa Cuatrecasas, Mwanashirika la Watawa wa Bikira  Maria wa Mlima Karmeli; alizaliwa huko Sant Joan les Fonts (Uhipania) tarehe  16 Juni 1878 na kifo chake huko Elda (Uhispania) tarehe 27 Novemba 1918;  Maria Addolorata wa Moyo uliochomwa , (jina la ubatizo Maria Luciani), Mtawa wa Shirikwa la watawa wa Mateso ya Yesu Kristo; alizaliwa huko Montegranaro (Italia) tarehe 2 Mei 1920 na kifo chake huko  Teramo (Italia) tarehe 23 Julai 1954; na Lodovico Coccapani, mlei wa Shirika la Wafrasiskani wasekulari , alizaliwa , huko  Calcinaia (Italia) tarehe 23 Juni  1849 na kifo chake tarehe  14 Novemba 1931.

09 November 2018, 15:41