Zawadi ya toleo la Tamasha la 10 kwa Waandishi wa Habari wa Mediterrania!
Sr. Angela Rwezaula - Vatican
Waliokuwa bora katika utoaji taarifa za kitaifa na kimataifa kwa kile kinachotokea katika Mediterrania na historia ambazo zinasaidia, si tu kubaki tofauti bali, ni kujua vema kila ambacho kinatukia katika dunia hata kutoa nafasi ya kufakari kwa dhati. Na ndiyo zawadi inayotolewa kwa karibu ya miaka 10 mfululizo wa Mashindano ya Tamasha wa Waandishi wa Habari wa Mediterranea wa Otranto, ambao kwa mwaka 2018 imekwenda sambamba na Kipeo kikubwa ambacho kinaikumba Bahari ya Mediterranea: kwa mfano wa vita vya Siria,Yemen, Libia Iraq, tishio la kigaidi kimataif, majanga ya wahamiaji na mambo mengi yaliyo karibu na sisi, kwa mujibu wa Lino Patruno , mhusikia Mkuu wa habari katika kujenga amani.
Nafasi ya habari
Kutokana na hili, nafasi ya habari imepata fursa ya kufanya mjadala katika tamasha ambalo limehitimishwa; Katika viwanja na fukwe za Otranto, wamezungumzia kwa kina juu ya mfumo wa habari za kugusi ( fake news); hata za kutoa habari mbaya, na uchakachuaji wa habari, pamoja na nafasi ya vyombo vya habari vya kijamii. “Waandishi wa habari hawatoi suluhisho la matatizo yaliyopo, lakini wanao uwajibu mkubwa”, amesisitiza Bwana Stefano Pilli Kaimu Mkurugenzi wa Gazeti la Ansa ambapo katika Mashindanuo amepokea naye tuzo kutokana na kuandaa mpango wa Habari za wahamiaji, yaani (Infomigrants) ambalo ni huduma inayotolewa katika lugha mbalimba kwa ajili ya wahamiaji zinazotolewa na Gazeti la Ansa , kwa ushirikiano wa Vyombo vya habari vya Ufaransa na Deutsche Welle (DW) pia hata Paolo Messa mwanzilishi wa Portale “Fomiche”.
Washindi katika sekta tatu za mashindano
Washindiwamegawanyika katika sekta tatu inayohusu mada ya amani na wahamiaji; Sehemu nyingine inayohusu Mediterranea na haki ambazo hazitambuliki; na Sehemu ya tatu inahusu Ugaidi wa kimataifa.
Ubunifu wa teknolojia wa Vatican News
Hata hivyo kuna aina nyingine ya zawadi iliyotolewa nje ya mashindano ambaye imekwenda kwa Vatican News kutokana na ubunifu wa kiteknolojia, kwa ajili ya video zilizoonesha wakati wa kutoa zawadi, ambazo mwezi Desemba mwaka jana walionesha juu ya kazi ya mageuzi ambayo vyombo vya habari Vatican vilikuwa vikiendelea kujikita na mchakato huo kwa kusindikizwa na baadhi ya mabaraza ya kipapa. Aliye onesha na kupokea zawadi hiyo na Massimiliano Menichetti mratibu wa Habari kwa lugha nyingi Vatican akiongozana na kikundi cha wanahabari wa Vatican na waandishi wengine, kwa upande wa Video Benedetta Capelli, Cecilia Seppia, Emanuela Campanile,pamoja na wahaudumu wa Papa, Cesare Cuppone.
Na katika sababu zilizosukuma ubunifu wa lazima leo hii kusimulia matendo ambayo yanaendelea kwa ajili ya vyo vya habari Vatican ni ile ya kuwa makini zaidi kwa masuala yanayo husi abinadamu, katika haki, na mada nyingi zinzohusu amani na mazungumzo