Tafuta

Orodha ya washiriki wa Sinodi ya Maaskofu kuhusu vijana imetolewa Orodha ya washiriki wa Sinodi ya Maaskofu kuhusu vijana imetolewa 

Orodha ya watakao shiriki Sinodi XV ya maaskofu kutolewa!

Mwenyekiti wa Tume ya Mawasiliano ni Paolo Riffini, Rais wa Baraza la Kipapa la Mawasiliano na katibu ni Padre mjesuit Antonio Spadalo , mkurugenzi wa Gazeti la Civilta' Cattolica, ni kati ya washiriki kwenye orodha ya watakao udhuria Sinodi ya Maaskofu kuhusu viijana itakayo anza tarehe 3 -28 Oktoba 2018

Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Tarehe 15 Septemba 2018, Shirika la Habari Vatican limetoa orodha ya watakao shiriki Sinodi XV ya maaskofu ambayo itaanza mjini Vatican tarehe 3 Oktoba 2018 juu ya mada “ Vijana , imani na maang’amuzi ya miito.

Orodha hiyo inaanza na Papa Francisko, Mwenyekiti wa Sinodi ya Maaskofu, Katibu Mkuu, Kardinali Lorenzo Baldisseri, na wenyeviti wanne wawakilishi: Kardinali, Louis Raphaël I Sako, Patriaki wa Babilonia wa Wakaldayo na Mkuu wa Sinodi ya Kanisa la Wakaldayo (Iraq); Kardinali  Desiré Tsarahazana, Askofu Mkuu wa Toamasina (Madagascar); Kardinali  Charles Maung Bo, Askofu Mkuu wa Yangon (Myanmar); Kardinali John Ribat, Askofu Mkuu wa Port Moresby (Papua Nuova Guinea).

Orodha inafuata watoa mada wakuu Kardinali Sérgio da Rocha, Askofu Mkuu wa Brasilia na rais wa Baraza la maaskofu wa  Brazil, pia Makatibu wawili maalumu: Padre Giacomo Costa, Mkurugenzi wa Gazeti (Aggiornamenti Sociali")Sasisho Kijamii,  Rais wa Chama cha Utamaduni  cha Matakatifu Fedele na Makamu rais wa Chama cha Carlo Maria Martin, na Padre msalesiani, Rossano Sala, Profesa wa Masuala ya kichungaji ya vijana katika Chuo Kikuu cha Wasalesiani na Mkurugenzi wa Gazeti  la "Note di Pastorale Giovanile". Yaani masuala ya kichungaji kwa vijana.

Pia kuna Tume  kwa ajili ya mawasiliano akiwa ni Bwana Paulo Ruffini, Rais wa Baraza la Kipapa la Mawasialiano, na Katibu wake Padre Antonio Spadaro Mkurugenzi wa Gazeti la Civilta Cattolica. Rais wa Tume kwa ajili ya mijadala Kardinali Giuseppe Versaldi, Rais wa Baraza la Kipapa la Elimu Katoliki.

Orodha inaendelea kuonesha,  Wajumbe wawili kutoka katika tume hiyo, Askofu Mkuu  Charles Jude Scicluna, wa  Malta, na Askofu Godfrey Igwebuike Onah, wa jimbo la  Nsukka nchini Nigeria.

Baadaye inafuata orodha kamili ya Mapadri wa Sinodi kutoka dunia nzima,  walio changuliwa na ofisi, wahudumu, wasikilizaji, wakiwa ni wake kwa waume, washauri, wasaidizi na wajumbe wengine  ndugu kutoka Makanisa mbalimbali ya kikristo. Katibu msaidizi wa Sinodi ya  maaskofu ni Askofu  Fabio Fabene, wajimbo la  Montefiascone.

 

 

17 September 2018, 15:46