Tafuta

Askofu  Bernadito Auza, Mwakilishi wa kudumu wa Vatican katika Ofisi za Umoja wa Mataifa New York Askofu Bernadito Auza, Mwakilishi wa kudumu wa Vatican katika Ofisi za Umoja wa Mataifa New York 

Lazima kuvalia njuga sheria za kulinda viumbe baharini na visiwa

Askofu Mkuu Bernardito Auza Mwakilishi wa Kudumu wa Vatican katika Ofisi za Umoja wa Mataifa zilizoko jijini New York, Marekani wakati wa kutoa hotuba yake kwenye kikao kuhusu mwelekeo wa dunia kwa ajili ya mabadiliko ya tabia nchi, kikao kilichoanza tangu tarehe 4- 7 septemba 2018

Sr. Angela Rwezaula - Vatican

Mataifa yanalazimishwa kushirikishana kuwajibika katika kukabilishana na mazingira kwenye shughuli zao kisayansi na kiuchumi ili kuzuia hatari ya uwezekano wa majanga  hasa katika mfumo wa kuishi maeneo ya bahari na nje na nchi kavu. Hayo ni maelezo  ya Askofu Mkuu  Bernardito Auza  Mwakilishi wa Kudumu wa Vatican katika Ofisi za Umoja wa Mataifa zilizoko jijini New York, Marekani wakati wa kutoa hotuba yake kwenye kikao  kuhusu mwelekeo wa dunia kwa ajili ya mabadiliko ya tabia nchi, kikao kinacho endelea ambacho kilianza tangu tarehe 4- 7 septemba 2018.

Hii inatakiwa kubadili mtazamo juu ya haki kwa kujikita katika mtazamo wa uwajibikaji. Ndiyo fundo la suala la kukabiliana katika wakati endelevu wa rasilimali za bahari, ambazo zinawekwa bayana na Askofu Mkuu Bernadito Auza wakati wa kutoa hutuba yake mjini New York. Ni mkutano ambao unajikita kutafuta kuweka makubaliano ya kisheria katika matumizi ya kulinda mazingira endelevu ya viumbe wanaoishi majini na nchi kavu kutokana na msingi wa Mkataba wa Kimataifa juu ya haki ya bahari.

Hitaji la mkakati wa muda mrefu

Akiendelea na hotuba yake anasema, kwa kuzingatia umuhimu wa haki katika ngazi ya ulimwengi ili kuthibiti uharibifu wa ardhi, na kama Papa Francisko anavyosisitiza katika Waraka wake wa Laudato Si, Vatican inatibitisha kwamba sheria mpya za kulinda mazingira na zisiwe  chagizo cha kimaadili tu, bali hata cha kupata suluhisho la maisha kutokana na hali mbaya na ambayo inahitaji matendo ya dhati ya haraka na dharura. Ili kuweza kufikia lengo hilo la kushirikishana na kuhifadhi matumizi endelevu ya viumbe baharini , ni lazima kuwa na mkakati wa muda mrefu kwa ajili ya upyaisho ulio msafi na maendelo ya bahari na visiwa. Katika makubalino yanayo tazama shughuli za kisayansi na biashara, Askofu Mkuu Auza anashauri kwama, siyo kutuliza tu makonakona  ya sasa katika mkataba wa sheria, wala kutoa ahadi ya mipango iliyopo katika sehemu, sekta na kanda, badala yake ni kuzuia kabisa ulazima wa michakato ya makubaliano ya dunia kila mara inapogunduliwa rasilimali mpya au shughuli za kibiashara zisifanyike katika maji na mipaka yake.

Njia za kuhamasisha kwa matendo

Askofu Mkuu Auza anatoa mapendekezo ambayo yanaweza kuwa ya dhati  na kwamba hayo  yanaweza kuunganishwa katika mantiki sita. Hawali ya yote ni ule umakini wa bahari na idadi kubwa ya mitindo ya maisha,ikiwa ndiyo kiini cha kila mjadala juu ya rasilimali na faida kiuchumi na kupelekea ulazima wa mataifa na wazalendo wake. Kwa maana hiyo ni kuchanganua aina mbili za kuhifadhi na matumizi endelevu pamoja na kukuza ushirikiano wa Kiteknolojia  na utafiti juu ya rasilimali za visiwa, kwa namna ya pekee maji ili kuwa na mwelekeo unaofaa katika maendeleo endelevu kwa kusisitizia zaidi  juu ya mahusiano ya fedha na kuzingatia vema ubora wa mantiki za kibiashara.

Kutofautisha hata rasilimali na thamani yake kiuchumi kwa haraka kama vile madini ambayo yanatokana na thamani yanye  nguvu kama vile: upepo na nguvu ya jua (Sola system). Na hatimaye ni kutofautisha kwa mfano kwa lengo la utafiti wa kisayansi baharini au kuogelea,shughuli  ambayo inapaswa kuthibitiwa  na matumizi hayo lazima yawe yanathibitiwa kikamilifu. Mataifa lazima  yafanye tathimini kwa ajili ya mazingira, lakini hata majanga ambayo yanaweza kutukia, kwa kubuni mbinu ya kuzuia hatari katika maeneo ambayo yako mbali na forodha zao.

Utetezi wa maisha ndiyo yawe katika mstari wa kwanza

Umuhimu wa rasilimali za binadamu, anatoa ushauruki kuwa ujumu wa blu,, ambao unajikita katika mitindo ya biashara kwa namna ya kupatanisha mazingira endelevu, na shughuli za kazi , ziko tayari katika kukua kwa wakati huu. Shughuli yetu kubwa leo ni kutangulia mabadiliko haya. Kutoa kipaumbele cha maisha katia mitindo  yake yote na kuweka nyumba yetu ya pamoja kuwa mstari wa mbele.

06 September 2018, 15:19