Tafuta

Papa Francisko katika harakati za kutetea na kulinda watoto waathirika Papa Francisko katika harakati za kutetea na kulinda watoto waathirika 

Papa:Kanisa litoe kipaumbele kwa waathirika wa manyanyaso !

Tamko la Mkurugenzi wa vyombo vya habari Vatican Bwana G.Burke juu ya ripoti kuhusu vitendo vya unyanyaswaji, vilivyosabaishwa na Kanisa la Pennsylvania, ni aibu na uchungu na Baba Mtakatifu yupo kwa upande wa waathirika. Kanisa linataka kuwasikiliza ili kuweza kung’oa janga hili la kutisha ambalo linaharibu maisha ya wasio na hatia

Sr. Angela Rwezaula - Vatican

Mbele ya ripoti ilitolea kwa umma huko Pennsylvania mapema wiki hii, yapo maneno mawili ambayo yanaweza kujieleza kulingana na majaribu mbele ya majanga ya kihalifu na kutishia ambayo ni aibu na uchungu. Hayo ni  maneno kwa mujibu wa  Mkurugenzi wa Habari za Vatican Bwana Greg Burke.

Bwana Burke akiendelea na taarifa hiyo kwa vyombo vya habari amesisitiza kwamba “Vatican inafikiria kwa umakini mkubwa wa  kazi ambayo imefanyiwa na upelelezi  wa  chombo cha Investigating Grand Jury  huko Pennsylvania na ripoti kamili  (Interim Report) iliyoitolewa. Ktuokana na ripoti hiyo, Vatican inahukumu vikali manyanyaso hayo juu ya watoto.  Na waliofanya manyanyaso hayo hata wotewalioandikwa katika ripoti hiyo wanahukumiwa na kimaadili kupewa onyo kali.  Kwa maana matendo hayo yamesaliti matumaini na kuiwaibia waathirika hadhi yao na imani yao”

“Kanisa lazima lifunze kutokana na mafundisho makali  ya wakati uliopita na lazima kuwajibika kwa wale ambao wamesababisha manyanyaso, hata kutenda. Sehemu kubwa katika ripoti inatazama manyanyaso yaliyotokea wakati wa miaka kabla ya 2000. Kutokana na kutopata kesi nyingine baada ya mwaka 2002, hItimIsho  la uchunguzi wa Grand Jury, wamekuwa makini katika upelelezi uliotanguliwa na ambao wameonesha jinsi gani  kuna mabadiliko ya Kanisa Katoliki Marekani na jinsi gani wameweza kupungza matukio haya ya manyanyaso yaliyosababishwa na makleri. Vatican inawatia moyo bila kuchoka hayo mageuzi na usimamizi kwa ngazi zote za Kanisa Katoliki katika kuhakikisha ulinzi wa watoto na watu wazima waliodhulika. Zaidi ripoti inasisitizia juu ya umuhimu wa kutii sheria za raia wakiwemo ulazima wa kutoa ripoti kesi za nyanyaso dhidi ya watoto”

Bwana Burke anahitimisha akithibitisha kuwa, Baba Mtakatifu Francisko anatambua vema jinsi gani uhalifu huo umeweza kutingisha na kudhoofisha imani na roho ya waamini, anatoa wito wa kufanya kila juhudi ili kuunda mazingira salama kwa ajili ya watoto na watu wazima waliodhulika  katika Kanisa na katika jamii nzima. Waathirika  lazima watambue kuwa, Baba Mtakatifu yuko  katika upande wao. Na wote walioteseka ndiyo wa kupewa kipaumbele, pia Kanisa linataka kuwasikiliza ili kuweza kung’oa janga hili la kutisha na ambalo linaharibu maisha ya wasio kuwa na hatia”

17 August 2018, 15:35