Askofu Mkuu Dagoberto CAMPOS SALAS balozi wa kitume - Gambia
Sr. Angela Rwezaula - Vatican
Tarehe 17 Agosti 2018 Baba Mtakatifu Francisko amemteua Balozi wa kitume katika nchi ya Gambia Askofu mkuu Dagoberto CAMPOS SALAS wa Forontiniana, ambaye alikuwa Balozi wa kitume nchini Liberia.
Askofu Mkuu Dagoberto CAMPOS SALAS alizaliwa Puntarenas, kisiwani Costa Rica kunako tarehe 14 Machi 1966 huko Campos Salas. Alipata daraja Takatifu la Upadre mnamo tarehe 22 Mei 1994 na mwenye uzamivu wa Shahada ya Sheria.
Alianza shughuli za kidiplomasia Vatican tangu tarehe 1 Julai 1999. Katika shughuli hiyo ameweza kushika nafasi ya ubalozi wa kitume Vatican katika nchi za Sudan, Chile, Sweden, Uturuki, Mexico na wakati wa kuteuliwa kwake alikuwa ni Balozi wa kitume huko Tilarán-Liberia. Anafahamu vizuri ligha ya kihispania, kingereza na kiitaliano.