Tafuta

Papa Francisko akitazama filamu ya  'Freedom on Fire: Ukraine's Fight for Freedom' Papa Francisko akitazama filamu ya 'Freedom on Fire: Ukraine's Fight for Freedom'  (ANSA)

Papa:ukatili na maumivu katika Ukraine,karibu na watu ambao wanatetea utambulisho wao

Papa Francisko alihudhuria onesho la filamu ya mkurugenzi Afineevsky "Freedom on Fire"ambayo inasimulia utisho wa vita tangu uvamizi wa Urussi Februari 24, 2022.Tukio hilo lilifanyika alasiri mjini Vatican,katika hafla ya kuadhimisha miaka kumi ya Mapinduzi ya Utu.Papa aliwasalimia na kuwabariki waliokuwepo,miongoni mwao ni Myahudi mmoja New Jersey.

Vatican News

Jioni ya  Jumanne tarehe 21 Novemba 2023,  Baba Mtakatifu Francisko alifika kwenye Ukumbi mpya wa Sinodi saa 12.30, wakati wa  tukio la onesho ya filamu yenye kichwa, “Freedom on Fire: Ukraine’s fight for freedom,” yaani Uhuru juu ya moto. Ukraine inapambania huru, ya mtunzi Evgeny Afineevsky, ambayo ilifanyika mbele ya baadhi ya wanadiplomasia, miongoni mwao akiwemo Mwanadiplomasia, Balozi wa Ukraine anayeakilisha nchi yake mjini Vatican, wageni wa  Italia na wageni wengine wa  kimataifa. Ni habari zilitotolewa na Msemaji wa Vyombo vya habari mjini Vatican, Dk. Matteo Bruni.

Papa akiwasalimia walioshiriki kutazama filamu kuhusu Ukraine yapambania uhuru wake
Papa akiwasalimia walioshiriki kutazama filamu kuhusu Ukraine yapambania uhuru wake

Kwa mujibu wa Msemaji huyo kwa waandishi alisema kuwa Papa alikaa hadi mwisho wa onesho hilo baada ya kimya cha dakika moja katika sala kwa ajili ya waathiriwa  wa  mzozo huo na  hotuba fupi ya mkurugenzi, alihutubia baadhi ya maneno ya salamu kwa washiriki, na kuwashukuru kwa kutoa ushuhuda huo.

Washiriki wa kutazama filamu
Washiriki wa kutazama filamu

Kwa njia hiyo maumivu mengi  hayo alisema tena"Vita ni kushindwa kila wakati" alikumbuka  kuwa na sisi, ambao tumeona ukatili huo, watu hawa wanaotetea utambulisho wao, lazima tuwe karibu na mateso mengi na kuwaombea watu hawa, tuombe amani ifike". Kabla ya kuondoka, Baba Mtakatifu kwa hiyo aliwasalimia baadhi ya wageni mmoja mmoja na kisha akarejea Nyumba ya Mtakatifu  Marta.

Papa alitazama filamu kuhusu amteso ya Ukraine
22 November 2023, 10:07